Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Finance Wizara ya Fedha 54 2023-09-01

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza:-

Je, hatua zipi zimechukuliwa kuhusu Itifaki ya Forodha kati ya Tanzania na DRC kujiunga na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, DRC imeshawasilisha hati ya kukubali kutekeleza Itifaki ya Umoja wa Forodha (Instrument of Ratification) kwa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Aidha, DRC inaendelea na mchakato wa kufanya marekebisho ya sheria zake za ndani ili ianze kutumia Sheria ya Pamoja ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukamilisha mchakato huo, DRC itafanya vikao na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kukubaliana kuhusu utaratibu wa utekelezaji wa mpango wa utekelezaji (road map) ili kujua lini itaanza utekelezaji wa Itifaki ya Forodha ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, ahsante.