Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 82 2021-11-11

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: -

Je, ni Ranchi ngapi nchini zimeshawapokea wafugaji na kuwapatia nafasi ya kufuga kwenye Ranchi hizo kama Serikali ilivyotoa maelekezo?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Costantino Mwakamo Mbunge wa Kibaha Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) imetekeleza maelekezo ya Serikali kwa kutenga jumla ya vitalu vya muda mrefu 116 katika Ranchi 11 za NARCO na kuzikodisha kwa wafugaji wadogo 116. Ranchi hizo ni Kikulula (Kagera) vitalu 2, Mabale (Kagera) vitalu 7, Kagoma (Kagera) vitalu 18, Kitengule (Kagera) vitalu 10, Missenyi (Kagera) vitalu 11, Mkata (Morogoro) vitalu 7, Dakawa (Morogoro) vitalu 2, Mzeri Hill (Tanga) vitalu 9, Usangu (Mbeya) vitalu 16, Kalambo (Rukwa) vitalu 13 na Uvinza (Kigoma) vitalu 21. Jumla ya eneo la vitalu hivi ni hekta 322,525.

Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kutatua migogoro ya wakulima, wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi nchini hasa baada ya wafugaji kuondolewa kwenye hifadhi za misitu na mapori ya akiba, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) ilianzisha utaratibu wa kugawa vitalu vya muda mfupi ambapo jumla ya vitalu 128 vimekodishwa kwa wafugaji wadogo 128 kutoka katika Ranchi 10 za NARCO. Ahsante sana.