Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 32 2021-02-04

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa kike katika Shule za Msingi Birise na Donsee ambazo hazina walimu wa kike?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, asante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Yusuph Majala, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya ukosefu wa walimu wa kike katika Shule ya Msingi Birise na Donsee zilizopo katika Halmashauri ya Chemba, Mkoa wa Dodoma.

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Chemba imempeleka mwalimu mmoja wa kike katika Shule ya Msingi Donsee wakati ikiendelea na utaratibu wa kukamilisha kumpeleka mwalimu mwingine wa kike katika Shule ya Msingi Birise.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikijiandaa na mpango wa ajira na mgawanyo wa walimu wapya kwa Halmashauri zote nchini, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inazielekeza Halmashauri zote nchini kufanya msawazo wa walimu wa shule za msingi na sekondari kwa kuzingatia jinsia.