Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 9 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 115 2018-02-09

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-
Wananchi wa Wilaya ya Chunya wameanza kujenga uwanja wa michezo wa kisasa wa Wilaya.
Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia ujenzi huu ili ukamilike haraka?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya Maendeleo ya Michezo ya mwaka 1995 kifungu cha 5.1.8(b) (vi) inaelekeza wajibu wa mamlaka ya Serikali za Mitaa kushirikiana na wananchi katika kujenga, kulinda na kutunza miundombinu ya michezo ikiwemo viwanja vya michezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa ujenzi wa uwanja wa michezo wa Chunya unatekelezwa kwa kuzingatia sera ya michezo ikisimamiwa na Serikali kupitia Halmashauri ya Chunya kwa ushirikiano wa karibu na wananchi pamoja na wadau. Mradi huo unaotarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni nane umetumia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 100 zilizotolewa na Hamashauri ya Wilaya ya Chunya katika mwaka huu wa fedha 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Seriakli kupitia Halmashauri ya Chunya imetenga kiasi cha shilingi milioni 50 kwa ajili ya kuendelea na hatua mbalimbali za mradi wa ujenzi wa uwanja huo wa michezo.