Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 04 2018-01-30

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-
Tatizo la uhaba wa watumishi katika sekta ya afya kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Geita ni kubwa sana.
Je, Serikali ina mkakati gani wa dharura wa kuliondoa tatizo hilo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer


NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu wali la Mheshimiwa Lolesia Jeremiah Bukwimba, Mbunge wa Busanda kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina mahitaji ya watumishi wa sekta ya afya 465 ambapo waliopo ni 235 na upungufu ni 240. Upungufu huu umetokana na sababu mbalimbali ikiwemo uhamisho, vifo, kustaafu pamoja na zoezi la Kiserikali la kuondoa watumishi hewa na wale waliokuwa na vyeti fake. Hata hivyo, baada ya kukamilisha mazoezi hayo, Serikali imeanza kutoa vibali vya kuajiri kada mbalimbali ikiwemo kada ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mgao wa watumishi wa nchi nzima mwaka 2017, Halmashauri ya Wilaya ya Geita ilipata jumla ya watumishi 22 kati yao ni madaktari wawili. Watumishi hao wote wameripoti kwenye vitu na wanaendelea na kazi. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2018/2019, Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetenga katika bajeti na kuomba kibali cha kuajiri watumishi 121 katika sekta ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha Halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya kuajiri wataalam zaidi ili kutatua changamoto ya uchache wa watumishi katika wilaya hiyo.