Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 58 2024-02-02

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha Watanzania wote wanajua kusoma na kuandika?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kulingana na ripoti iliyotolewa na NBS, kwa sensa ya mwaka 2022 Tanzania imefikia kiwango cha asilimia 83 cha kujua kusoma na kuandika miongoni mwa watu wazima (miaka 15 na kuendelea), ikiwa ni ongezeko la asilimia 6.3 kutoka asilimia 78.1 cha sensa ya mwaka 2012.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha Watanzania wote wanajua kusoma na kuandika, Serikali imeendelea kutekeleza afua mbalimbali ikiwemo kuondoa vikwazo vya kupata elimu kama vile kutolewa kwa elimu ya msingi bila ada, elimu ya lazima sasa kuwa ya miaka 10, kutekeleza programu zenye lengo la kuwafikia Watanzania waliokosa fursa za elimu. Kwa mfano, Elimu ya Watu Wazima na ujifunzaji endelevu, utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Kusoma pamoja na kutoa fursa kwa wanafunzi walioacha masomo kwa sababu mbalimbali kurudi shuleni na kuendelea na masomo (re-entry program) kupitia Waraka Na. 2 wa mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, pamoja jitihada hizo, Serikali imeendelea kuboresha huduma za maktaba nchini katika ngazi za mikoa, wilaya na shule, ikiwa ni pamoja na maktaba mtandao, ili kuwawezesha Watanzania wengi zaidi katika maeneo mbalimbali kupata huduma ya kusoma huko waliko.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kwa lengo la kuongeza fursa kwa Watanzania wengi zaidi kujiunga na Elimu ya Watu Wazima, nakushukuru.