Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 53 2024-02-02

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya maji katika vijiji 42 vya Jimbo la Momba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Momba lina jumla ya Vijiji 72 ambapo mpaka sasa vijiji 30 vinapata huduma ya Majisafi na Salama kupitia miradi ya maji ya bomba. Katika kuhakikisha vijiji vyote vinapata huduma ya maji, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imeendelea na utekelezaji wa miradi ya Maji katika vijiji 12 vya Muungano, Ipata, Ntinga, Chindi, Makamba, Naming’ongo, Yala, Isanga, Kalungu, Lwatwe, Samag’ombe na Kakozi kwa gharama ya shilingi bilioni 9.45. Utekelezaji wa miradi hiyo unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2024.

Mheshimiwa Spika, vilevile Serikali imeanza kazi ya utafiti wa maji chini ardhini na uchimbaji wa visima virefu katika vijiji 16 vya Mkutano, Nzoka, Chilangwi, Itumba, Miunga, Mfuto, Machimbo, Mpwinje, Njeleke, Isunda, Chafuna, Msungwe, Sante, Siliwiti, Chole na Mtungwa ambapo unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2024 kwa shilingi milioni mia sita. Kukamilika kwa uchimbaji wa visima hivyo kutawezesha usanifu wa miundombinu ya usambazaji, kufanyika katika mwaka wa fedha 2024/2025 na utekelezaji wake kuanza. (Makofi)