Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 48 2024-02-02

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa wodi za wagonjwa, nyumba za Madaktari, maabara na mortuary katika Vituo vya Afya vya Mwanhalanga na Negezi utakamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Jimbo la Kishapu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilipeleka shilingi milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wazazi lenye huduma za upasuaji wa dharura katika Kituo cha Afya Mwanhalanga na shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa majengo matano katika Kituo cha Afya Negezi, ambapo ujenzi umekamilika na majengo yanatumika.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uhitaji wa miundombinu mbalimbali ikiwemo wodi za kulaza wagonjwa, nyumba za watumishi, maabara na majengo ya kuhifadhia maiti katika vituo vya afya Mwanhalanga na Negezi, katika Halmashauri ya Kishapu.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya utekelezaji, ahsante.