Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 24 2023-11-01

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:-

Je, lini Serikali itatoa idhini kwa Makampuni binafsi kutoa elimu ya kujikinga na majanga ya moto kwa Wananchi na Taasisi nchini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa makampuni binafsi kushiriki katika shughuli za huduma ya zimamoto na uokoaji nchini, kama vile ufungaji wa mifumo ya kuzima moto, usambazaji na matengenezo ya vifaa vya kuzima moto kwa wananchi na taasisi. Serikali itafanya marekebisho madogo ya kanuni ya ukaguzi, tozo na cheti ya mwaka 2008 ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kutambua na kujumuisha makampuni binafsi katika utoaji wa elimu ya kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto kwa masharti na vigezo vitakavyowekwa na Serikali, nashukuru.