Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 20 2023-11-01

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESHTER E. MALLEKO aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuhusisha Majeshi ya Ulinzi na Usalama katika kulinda miradi mikubwa ya kimkakati?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alIjibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama ilivyoainishwa katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limeendelea kulilinda Taifa letu pamoja na Miradi Mikubwa ya Kimkakati kwa maslahi mapana ya Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kupitia Makao Makuu ya Jeshi imekuwa ikitoa wataalam mbalimbali wanaoungana na wataalam wa vyombo vingine vya Usalama ili kuhakikisha miradi ya kimkakati inakuwa salama wakati wote, nashukuru.