Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 16 2023-11-01

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itazilipa fedha Kampuni za Usambazaji wa Mbolea na Viuatilifu Mtwara?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Hasan Seleman Mtenga, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kulipa madai ya Kampuni na Mawakala wa pembejeo yaliyotokana na usambazaji wa pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea na viuatilifu kwa wakulima hapa nchini. Madai hayo ni pamoja na madai ya Kampuni na Mawakala waliosambaza pembejeo kwa mfumo wa ruzuku katika msimu wa 2015/2016 katika Mikoa 24 ya Tanzania Bara ukiwemo Mkoa wa Mtwara. Madai hayo yalifanyiwa uhakiki na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG). Hadi kufikia Septemba, 2023 kiasi cha shilingi 42,440,275,705.00 kimelipwa kwa Kampuni na Mawakala 307 wanaostahili kulipwa. Kati ya kiasi hicho, shilingi 679,750,000 zimelipwa kwa kampuni zinazohudumu Mkoa wa Mtwara.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika msimu wa 2021/2022 na msimu wa 2022/2023, Serikali iliratibu usambazaji wa tani 28,576.70 za sulphur, lita 4,181,824.50 za viuatilifu vya maji na mabomba 1,337 yenye thamani ya shilingi 156,325,550,300.00 kwa ajili ya wakulima wa korosho katika maeneo ya uzalishaji ikiwemo Mtwara. Kati ya kiasi hicho, Serikali imewalipa wazabuni kiasi cha shilingi bilioni 112.7, na deni lililobaki ni shilingi bilioni 43.5. Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha malipo ya madeni hayo.