Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 15 2023-11-01

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuelekeza taasisi zake kununua mashine na vipuri katika kiwanda cha Kilimanjaro Machine Tools?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) imekifanyia ukarabati mkubwa Kiwanda cha Kilimanjaro Machine Tools (KMTC) ikiwa ni pamoja na kujenga tanuri la kuyeyushia chuma (Foundry), ukarabati wa miundombinu ya kiwanda na utengenzaji wa mtambo wa kuweka utando katika bidhaa za chuma ili kuzuia kutu (hot dip galvanizing plant).

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kuwa taasisi zake zinazotumia bidhaa na vipuri vinavyozalishwa na KMTC zinaingia mikataba ya kununua mashine na vipuri kutoka KMTC, nakushukuru.