Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 10 2023-11-01

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itagawa Kata za Matiri, Litumbandyosi, Linda, Mkumbi, Litembo, Nyoni, Maguu na Langiro Wilayani Mbinga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa kuanzisha maeneo mapya ya utawala upo kwa mujibu wa sheria za Serikali za Mitaa Sura ya 287 na 288 pamoja na mwongozo wa uanzishwaji wa maeneo ya utawala wa mwaka 2014, Hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga inashauriwa kuanzisha mchakato wa maombi ya Kata za Matiri, Litumbandyosi, Linda, Mkumbi, Litembo, Nyoni, Maguu na Langiro kwa kufuata utaratibu ulioainishwa kwa kuanza na vikao vya ngazi za vijiji, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kisha kuwasilishwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kwa tathimini ya vigezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kwa sasa Serikali imetoa kipaumbele katika kuboresha na kukamilisha miundombinu msingi kwenye maeneo yakiutawala yaliyopo ili yaweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi na baadae kuendelea na maeneo mengine kwa kufuata taratibu na vigezo vilivyoainishwa, ahsante.