Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Natural hazards and Disasters Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 73 2023-11-06

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI aliuliza:¬-

Je, sababu zipi zimekwamisha ujenzi wa ukuta maeneo yanayoathiriwa na Bahari Nungwi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-¬

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Simai Hassan Sadiki, Mbunge na Mtumishi wa Wananchi wa Jimbo la Nungwi, najibu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Tabianchi katika maeneo mbalimbali ya ukanda wa fukwe wa Bahari ya Hindi. Lakini kutokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha zoezi la ujenzi wa ukuta wa Nungwi umechelewa lakini kwa sasa Serikali imepata fedha kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais imetenga fedha jumla ya shilingi milioni mia sita na hamsini kwa ajili ya kufanya tathmini ya awali ili kuwa na usanifu wa miundombinu itakayosaidia kurudisha ufukwe katika hali ya awali.

Mheshimiwa Spika, napenda nichukue nafasi hii kuwahimiza wananchi wa maeneo ya Pwani kuongeza jitihada za kupanda mikoko, kutofanya uchimbaji holela wa mchanga lakini pia kuhamasisha ulimaji na uvunaji wa mwani usiyoharibu fukwe. Aidha, Ofisi ya Makamu wa Rais na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar zitaendelea kushirikiana katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto za uharibifu wa mazingira katika maeneo mbalimbali, nakushukuru.