Parliament of Tanzania

Wachezaji wa Bunge Sports Club wawasili Sudan Kusini kushiriki Michezo ya Mabunge ya A. Mashariki

Wachezaji wa Timu ya Bunge Sports Club wamewasili Jijini Juba nchini Sudan Kusini kwa ajili ya kushiriki katika mashidano ya michezo ya 12 ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inayotarajiwa kuanza tarehe 25 Novemba hadi 2 Disemba 2022.

Awali Naibu Spika wa Bunge, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu aliwakabidhi Wachezaji hao bendera ya Taifa na Bunge kwa niaba ya Spika wa Bunge. Tukio hilo lilifanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.

Aidha akizungumza na Wachezaji hao kabla ya kuwakabidhi bendera Naibu Spika aliwaasa kudumisha heshima ya taifa pamoja na nidhamu wakati wote wa mashidano.

"Nendeni mkadumishe heshima ya taifa letu na mkalitangaze, kama taifa tuna fursa mbalimbali zikiwemo za utalii," alisema Naibu Spika.

Pia Naibu Spika aliwaambia wachezaji hao kwamba wanatarajiwa kurudi na vikombe katika michezo mbalimbali ambayo watashiriki.


Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's