Parliament of Tanzania

Kamati za Kudumu za Bunge zaanza kukutana Jijini Dodoma

Kamati za Kudumu za Bunge zimeanza kukutana Jijini Dodoma Jumatatu tarehe 8 Machi 2021 kwa ajili ya vikao vinavyotangulia kabla ya Mkutano wa Tatu wa Bunge uliopangwa kuanza tarehe 30 Machi, 2021.

Kwa mujibu wa ratiba Kamati hizo zitakuwa na shughuli zifuatazo;

i) Kupokea mapendekezo ya Serikali kuhusu Mpango, kiwango na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 kwa mujibu wa Kanuni ya 116(1) ya Kanuni za Kudumuza Bunge Toleo la Juni, 2020. Wabunge wote watahusika na shughuli hii;

ii) Kutembelea na Kukagua Utekelezaji wa Miradi iliyotengewa fedha kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ili kuzingatia masharti ya Kanuni ya 117(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Juni, 2020. Wajumbe wa Kamati za Kisekta watahusika na shughuli hii;

iii) Ziara za Ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za Umma kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa, Serikali Kuu na Taasisi za Umma ili kuzingatia masharti ya sehemu ya Nne ya Nyongeza ya Nane ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Juni, 2020;

iv) Uchambuzi wa taarifa za Uwekezaji uliofanywa na Serikali kupitia mashirika, taasisi na Kampuni ambazo Serikalii na Hisa pamoja na ziara ya kukagua shughuli za uwekezaji zilizofanywa na Serikali kupitia Mashirika, Taasisi na Kampuni ambazo Serikali ina Hisa. Wajumbe wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma watahusika na shughuli hii;

v) Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwa mujibu wa Kanuni ya 117(2) ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Januari, 2020. Wajumbe wa Kamati za Kisekta, Kamati ya Bajeti na Kamati ya Masuala ya Ukimwi watahusika na shughuli hii;

vi) Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Pili wa Bunge ili kutekeleza masharti ya kifungu cha 11 cha Nyongeza ya Nane ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Juni, 2020;

vii) Mashauriano kati ya Kamati ya Uongozi na Kamati ya Bajeti kuhusu masuala muhimu yatakayokuwa yamejitokeza kwenye Kamati za Kisekta wakati wa uchambuzi wa Taarifa za utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/20 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2020/21. Shughuli hii ni kwa mujibu wa Kanuni ya 117(5) na 117(6) ya Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Juni, 2020.


Hon. Job Y. Ndugai

Speaker of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

Member of the Parliament