Parliament of Tanzania

Kamati za Kudumu za Bunge katika vikao Jijini Dodoma

Vikao vya kawaida vya Kamati za Kudumu za Bunge vimeanza kufanyika tarehe 7 Agosti, 2023 Jijini Dodoma na vinatarajiwa kuhitimishwa tarehe hadi 25 Agosti, 2023. Vikao hivi vinafanyika kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano wa Kumi na Mbili wa Bunge utakaonza tarehe 29 Agosti, 2023.

Shughuli za Kamati katika kipindi hicho ni pamoja na: -


i) Uchambuzi wa Miswada miwili (2) ya Sheria utakaofanywa na Kamati mbili: Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria na Kamati ya Bajeti;

ii) Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa wakati wa Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge;


iii) Uchambuzi wa Taarifa za Hesabu zilizokaguliwa na CAG kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022;


iv) Uchambuzi wa Taarifa za Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa lengo la kuliwezesha Bunge kufuatilia ufanisi na tija kwa Mitaji ya Serikali kwenye mashirika mbalimbali na taasisi; na


v) Uchambuzi wa Taarifa za Utendaji za Wizara kwa lengo la kuliwezesha Bunge kutekeleza jukumu la kuisimamia na kuishauri Serikali.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's