Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je kuna Sheria ya Huduma ya Afya inayosimamia utoaji na upatikanaji wa huduma za afya?

Supplementary Question 1

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwakuwa suala la huduma ya mama na mtoto imekuwa na changamoto kubwa.

Je, ni kwanini sasa Serikali isiweke kanuni inayosimamia Sera ya Huduma ya Mama na Mtoto? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali nyeti na la msingi la Mheshimiwa Mbunge ni kwamba kwanza tukishaleta Sheria ya Bima ya Afya kwa wote tutakuwa tumemaliza mambo mengine yote mimi ninachomuomba Mheshimiwa Mbunge kwasababu tayari tumekuja kwenu na mmeona mchakato wetu unaoendelea wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote na unaendelea kwa sasa ikifika hapa Bungeni tuhakikishe tumetengeza sheria nzuri, utaratibu mzuri nataka kuwahakikishia haya matatizo yanayojitokeza kila siku tutakuwa tumeyatafutia suluhisho la kudumu.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je kuna Sheria ya Huduma ya Afya inayosimamia utoaji na upatikanaji wa huduma za afya?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kuna sheria inayo guide mama wajawazito na wagonjwa kwaajili ya kutibiwa. Je, nini upande wa pili wa Serikali kuhusiana na vituo vya afya ambavyo hakuna jengo la mama na mtoto mfano Kata ya Wazo ambapo kunatokea vifo vingi kutokana na kukosekana kwa jengo hilo? Ahsante sana.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge ni shahidi hapa kwamba kwa mwaka huu katika historia ya Tanzania kuliko wakati wote fedha nyingi zimepelekwa kwenye eneo la afya naniukweli kwamba hatutaweza kumaliza vyote kwa wakati mmoja lakini kwakweli hoja yako Mheshimiwa Mbunge niyamsingi, kimsingi basi shirikiana na halmashauri yako na hata leo tuandike vizuri tuhakikishe tunashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI iingie kwenye utaratibu na kama haijawahi kuingia kwenye utaratibu tuanze sasa mchakato litekelezeke lakini kwa chini ya Rais Samia Suluhu Hassan wala usipate wasiwasi na hilo.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je kuna Sheria ya Huduma ya Afya inayosimamia utoaji na upatikanaji wa huduma za afya?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wananchi wa Jimbo la Ushetu kwa kutumia nguvu zao wameweza kukamilisha zahanati saba; Zahanati ya Butibu, Zahanati ya Itumbo, Itebere, Makongoro, Manungu, Bugera na Misayo ambayo ni Zahanati tumeipa kwa jina la Eliasi Kwandikwa ambayo imejengwa kwa msaada wa Kampuni GTI na hiyo zahanati yenyewe tayari inavifaa tiba. Lakini sasa ni lini Serikali inatuletea vifaatiba na watumishi kwenye zahanati hizi ili wananchi waweze kupata matibabu yao maeneo ya karibu badala ya kuendelea kwenda zaidi ya kilometa 80 kupata matibabu.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwanza mimi na yeye ili tufanye mambo ambayo yanatekelezeka ametaja zahanati zenye tatizo cha kwanza awasiliane na Mganga Mkuu wa Wilaya yake kupitia Mkurugenzi ili walete mahitaji husika wa eneo hilo mimi na yeye tushughulikie hilo liweze kufanyika nanimuambie tu Mheshimiwa Mbunge pamoja na fedha ambayo Mheshimiwa Rais wetu ameshazipeleka MSD lakini kwenye manunuzi ya juzi ya fedha zile za UVIKO kununua vifaatiba kama X-Ray, CT Scan Serikali ime-save yaani imepata salio baada ya kununua kwa bei rahisi ime-save zaidi ya bilioni 17 na zote zinaelekezwa kwenye kununua vifaatiba na madawa kwaajili ya vituo vinavyoanzishwa.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je kuna Sheria ya Huduma ya Afya inayosimamia utoaji na upatikanaji wa huduma za afya?

Supplementary Question 4

MHE: AGNES HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pamoja na majibu ya Serikali naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Je, ni sheria ipi kati ya hizo sheria 30 inayosimamia wanawake wajawazito wakati wa kujifungua wanaopata huduma zisizoridhisha? Hilo ni swali la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na swali la pili; je, sheria hizo zinaruhusu malipo ya fidia kwa wagonjwa wanaopata huduma zisizoridhisha au zisizo na ubora zinazopelekea athari za kiafya au hata kifo? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nijibu swali la Mheshimiwa Agness Hokororo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa namna ambavyo anafuatilia namna wananchi wanavyotolewa huduma za afya katika eneo lake. Ni kweli kwamba kumekuwepo na mambo anayoyasema kwa maana ya huduma ya mama na mtoto lakini si tu sheria, sheria za nchi yetu, utaratibu wa nchi yetu na kanuni za Wizara ya Afya zinataka mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano wapate huduma bure lakini sasa tunapokuja kujibiwa vibaya, kujibiwa kwa masuala ya fedheha maana yake kuna sheria za kiutumishi ambazo zipo zimeonyesha watu wanaofanya mambo yanayofanana na hayo lakini kuna sheria za maadili ya kitaaluma ambayo mara nyingi anapopatikana mtu ambaye amekuwa akijibu vibaya akifanya nini wakati mwingine anapitishwa kwanza kwenye sheria za maadili ya kitaaluma anawajibika lakini anaachiwa vilevile sheria za kiutumishi zichukue mkondo wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kama mdau mkubwa kwenye eneo hilo endelea kutusaidia na kutusaidia kutengeneza ushahidi wa kutosha kuwapata watu wa namna hiyo ili waweze kushughulikiwa kulingana na taratibu na sheria, ahsante.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je kuna Sheria ya Huduma ya Afya inayosimamia utoaji na upatikanaji wa huduma za afya?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vituo vyetu vya afya kwenye Jimbo letu la Vunjo kuna uhaba mkubwa wa wahudumu lakini pia kuna wahudumu ambao wanataka kujitolea ili wasaidie na wenyewe wamesomea mambo hayo hayo ya ukunga nakadhalika na unesi lakini hawana kazi. Je, Wizara haioni umuhimu wa kuweka utaratibu wa kuwaruhusu hawa ambao wanataka wajitolee kusaidia kutoa huduma bure hata kama watalipwa kidogo na wananchi ili waweze kuchukuliwa? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza anachokisema Kimei ni kweli kipo na nimetembelea jimbo lake tumeliona hilo na ameshakieleza mara nyingi lakini sasa Mheshimiwa Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu alishaelekeza na tayari utaratibu, muongozo wa ajira ya kujitolea umeshatengenezwa kwa level ya Hospitali za Mikoa na kwenda juu. Sasa tunashirikiana na amesema atashirikiana na Mheshimiwa Bashungwa ili kutengeneza na utaratibu kwa kushuka chini tuone tunafanyaje hilo liweze kutekelezeka kwa urahisi lakini ni jambo jema sana kwasababu hata kwenye shule zetu tumeona kwamba kuna walimu wengi wanajitolea na wanasaidia sana watoto nayo kwenye afya tungetamani tuwe na jambo kama hilo lakini tulitafakari kwa kina kabla ya kutekeleza.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je kuna Sheria ya Huduma ya Afya inayosimamia utoaji na upatikanaji wa huduma za afya?

Supplementary Question 6

MHE. CONCHESTA LEONCE RWAMLAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Nchi yetu ni kutoa Huduma ya Afya bure kwa wazee lakini sera hii imekuwa haitekelezeki kwasababu hakuna sheria. Je, ni lini Serikali itatunga sheria ili kumbana mpeleka huduma na mtoa huduma ili sera hii iweze kutekelezwa sawasawa kwa wazee? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokisema Mbunge kipo sidhani kama tatizo ni sheria tatizo ni kwamba wazee kweli wamewekewa dirisha lao lakini wanapoandikiwa prescription na madaktari na baadhi ya vipimo wanapofika kwenye kufanya vipimo au kuchukua dawa wanakosa dawa husika na hilo ndiyo maana tunazungumzia suala la usimamizi wa dawa kwenye vituo vyetu na kuhakikisha dawa zipo kwenye vituo vyetu ambalo kwaweli kama Wizara ya Afya na TAMISEMI sisi wenyewe huku juu hatutaweza tunawaomba Waheshimiwa Wabunge, Baraza la Madiwani na Wakuu wa Wilaya wasimamie kwasababu kuna fedha nyingi zinakuja za Basket Fund na mambo mengine ambayo usimamizi ukifanyika tutapunguza tatizo kwa zaidi ya asilimia 80 lakini Mheshimiwa Mbunge tukishapitisha Muswada wa Bima ya Afya kwa watu wote maana yake kimsingi suala hilo tena alihitaji sheria suala hilo ni kwamba tutakuwa tumelitatua moja kwa moja, ahsante sana.