Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika baadhi ya Kata Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipongeze Serikali na hasa Engineer Kundo kwa majibu mazuri aliyoyatoa. Lakini nimpongeze pia kwa namna ambavyo amefanya ziara katika Jimbo langu na kuiona changamoto hii kubwa katika eneo langu. Sasa kwa kuwa kata saba kati ya kata tisa ambazo zilikuwa na changamoto na sasa Kata ya Somagedi na Mwasubi bado zina changamoto ya aina hiyo hiyo. Je, nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba maeneo haya yaliyo na changamoto ya mawasiliano ya simu na yenyewe yanafanyiwa kazi kwa haraka?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo Mbunge wa Kishapu Kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kata ambazo amezitaja Mheshimiwa Mbunge zina changamoto ya mawasiliano lakini kati ya kata tisa kata saba anaenda kupata mawasiliano. Na haya maeneo katika hizi kata saba zote yanapatikana katika kitabu chetu cha bajeti ukurasa wa 153 ukianzia namba 578 mpaka namba 584 zote ni Kata za Kishapu ambazo zinaenda kupata huduma ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaamini kabisa kwamba baada ya kukamilisha kata hizi saba basi kwa sababu utekelezaji hauwezi ukaenda kwa pamoja baada ya kukamilisha hizi basi tutaangalia uwezekano namna ambavyo tunaweza kuleta mawasiliano katika kata mbili ambazo zitakuwa zimebaki, nakushukuru.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika baadhi ya Kata Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kumekuwepo na mwingiliano mkubwa wa mawasiliano na minara ya Safaricom kwenye kata ambazo ziko mpakani kwa upande wa Tarime na Rorya. Na hii inapelekea gharama kubwa kwa watumiaji kwa maana inaingia kwenye roming lakini pia uhafifu wa mawasiliano. Sasa nilitaka kujua ni lini Serikali itahakikisha inapeleka minara toshelezi ili wananchi wa kule waweze kupata mawasiliano bila kuingia upande wa Kenya wanakuwa kama wako Kimataifa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko Mbunge wa Viti Maalum Kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa katika maeneo ya Wilaya ya Rorya pamoja na Tarime kuna changamoto ya mawasiliano na changamoto yenyewe ni kuingiliana. Vilevile Serikali kupitia mradi wetu wa special zone and boarders tayari maeneo hayo tumeyazingatia kuhakikisha kwamba mawasiliano yanaenda kuimarishwa ili kusiwepo na mwingiliano wowote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na tunaelewa kabisa mwingiliano unasumbua na unaingilia hata masuala ya kiuchumi na kiusalama. Serikali inajua hilo na inachukua juhudi mahususi kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto hiyo.

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika baadhi ya Kata Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, Jimbo la Mpwapwa lina changamoto kubwa sana ya mawasiliano na hasa katika Kata za Luhambi, Lupeta, Mlembule, chitemo na Ihondo. Je, ni lini Serikali itaweka minara ya mawasiliano ili kutatua tatizo hili?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mpwapwa Kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa maeneo mengi nchini bado yana changamoto ya mawasiliano. Lakini kwa maelekezo ya Ilani yetu ya Chama Cha Mapinduzi ni kweli maeneo ni makubwa lakini hatuwezi kuyatekeleza ndani ya mwaka mmoja. Na ndio maana tunapanga mpango wa mwaka mmoja, tunapanga na mpango wa miaka mitano tunaamini kabisa kwa kipindi ambacho kuanzia sasa mpaka 2025 maeneo mengi yatakuwa yamepata suluhisho la mawasiliano kwa ajili ya wananchi wetu, nakushukuru sana.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika baadhi ya Kata Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 4

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela Kata ya Sangabuye Kituo cha Afya hakuna mawasiliano. Kata ya Kayenze Kisiwa cha Bezi hakuna mawasiliano. Ni zaidi ya miaka minne sasa Serikali iliahidi kupeleka minara katika kata hizo. Je, ni lini Serikali itapeleka minara katika kata hizo ili wananchi wa kata hizo waweze kupata mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Furaha Mbunge wa Viti Maalum Kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya Sangabuye ni eneo ambalo liko pembezoni mwa Ziwa Victoria ambapo mwaka huu mwezi wa pili nilifanya ziara na nikajionea hali halisi. Na Serikali ilichukua juhudi mahususi za kuhakikisha kwamba tunatafuta mtoa huduma akajenge mnara. Na tayari mkandarasi wa kwenda kujenga mnara katika eneo la Sangabuye tayari ameshapatikana. Hivyo tunasubiri tu muda wa utekelezaji ukamilike na wananchi wa Kata ya Sangabuye na Kituo cha Afya kilichopo pale waendelee kupata mawasiliano na vilevile wakinamama ambao wanatakiwa kulipa kwa kutumia M-pesa na Tigo-pesa basi haya mambo yote yaweze kwenda bila kuwa na shida yoyote, ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu katika baadhi ya Kata Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 5

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwenye Wilaya Kyerwa mwaka 2020/2021 kwenye bajeti tulitengewa minara saba na Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika Kyerwa ukatuahidi minara hiyo itajengwa lakini mpaka leo minara hiyo haijajengwa na wananchi wanaendelea kupata adha?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Bilakwate Mbunge wa Kyerwa Kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nilifika katika kata hizo na katika jimbo la Mheshimiwa Mbunge. Vilevile labda nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge ni kwamba tunapotangaza tender na mtoa huduma akapatikana maana yake yeye anaingia sasa kwenye kutafuta mkandarasi ambaye anaenda kumjengea minara hiyo. Na sasa tayari watoa huduma washatujulisha kwamba wako katika mchakato wa kuhakikisha kwamba mkandarasi anapatikana kwa ajili ya kwenda kujenga ile minara. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo lakini utekelezaji wa Serikali pale inapoahidi ni lazima ahadi yake itatimizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.