Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukiendeleza Chuo cha Hali ya Hewa kilichopo Kigoma ili kiwe Chuo Kikuu kishiriki cha Dar es Salaam na kiweze kutoa taaluma nyingine?

Supplementary Question 1

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, andiko la TMA kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni latokea mwaka jana mwaka wa 2021; na sasa tunakwenda kukaribia mwaka wa 2022. Nilitaka commitment ya Serikali kujua kwamba hatua hii inaweza ikakamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu, jambo hili litasaidia katika kuleta maendeleo ya wananchi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, mmejipangaje kuendelea na maboresho wakati mkisubiri maamuzi yale ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shabani Ng’enda, Mbunge Kigoma Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna ya kipekee kufuatilia Chuo hiki cha Hali ya Hewa pale Kigoma jimboni kwake.

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza anasema maandiko yalianza tangu mwaka 2021; kimsingi maandiko tumeandika mwaka huu na tumepeleka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tarehe 14 Aprili, 2022 lakini mwaka jana tulianza mazungumzo na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hivi sasa tunavyosema tulitegemea Seneti itakapokaa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ndipo tupate mrejesho pengine ndani ya miezi miwili ijayo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili anataka afahamu tumejipangaje namna ya kuboresha chuo hiki. Ni kweli kwamba chuo hiki ni mkombozi mkubwa katika Mamlaka ya Hali ya Hewa na chuo ni kimoja na Serikali kupitia bajeti zake mwaka wa fedha 2021/2022 tulitenga kiasi shilingi milioni 450 na tumejenga majengo pale kwa maana ya madarasa, maabara pamoja na computer room ama computer lab. Lakini hata hivyo, mwaka wa fedha na Waheshimiwa Wabunge mlitupitishia hapa tumetenga kiasi cha shilingi bilioni moja kwa ajili ya kujenga jengo la utawala, na tunahakika mwakani chuo hiki kitaboresha zaidi.

Name

Bakar Hamad Bakar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukiendeleza Chuo cha Hali ya Hewa kilichopo Kigoma ili kiwe Chuo Kikuu kishiriki cha Dar es Salaam na kiweze kutoa taaluma nyingine?

Supplementary Question 2

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ninataka kujua ni mpango upi wa Serikali kuweka miundombinu shindani kwenye Chuo hiki cha Hali ya Hewa Kigoma; hasa ukizingatia kwamba chuo hiki kwa nchi za Afrika ni nchi chache sana ambazo zinatoa taaluma hii na sisi kuweza kulitumia hilo soko la kuweza kupokea wanafunzi kutoka nchi mbalimbali Afrika? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bakar Hamad kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali tumejipanga vyema kukiboresha chuo hiki ili kiwe shindani katika nchi za Afrika Mashariki na Kati na ukizingatia kwamba hiki ni chuo pekee kinachotoa elimu hii ya hali ya hewa; na kwa msingi huo tumeingia makubaliano na Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT) ili kianze kutoa elimu ya TEHAMA lakini zaidi ya yote kwa sababu pia Chuo chetu cha NIT kitaanza kutoa mafunzo ya urubani na mafunzo ya urubani yanaendana na hali ya hewa. Kwa hiyo, hata hiki pia kitakuwa sehemu ya hayo mafunzo; na zaidi ya yote pia chuo chetu tunakitangaza hata nchi jirani kwa maana ya Rwanda pamoja na Burundi, ahsante.