Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuwaendeleza vijana wanaomaliza kidato cha nne na kupata daraja la nne au sifuri?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mimi nataka kujua tu, Serikali imeweka mkakati gani wa kuondokana na hili daraja sifuri? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mussa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyozungumza katika swali lililopita, suala la ufuatiliaji au suala la elimu ni lazima pande zote ziweze kushiriki, kwa maana ya mwanafunzi mwenyewe, ni lazima atengeneze mkakati wa namna gani anaweza kujifunza na kuhakikisha kwamba anafaulu kwenye masomo yake. Pia kuna sehemu ya walimu na vilevile kuna sehemu ya wazazi. Kwa hiyo, sisi kama Serikali jukumu letu kubwa ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na miundombinu wezeshi ya kumwezesha mwanafunzi kuweza kusoma na kupata elimu yake sawa sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile lazima tupeleke walimu wa kutosha kuhakikisha kwamba masomo yote yanafundishwa kwa vipindi vyote kwa wakati, kwa maana ya kutekeleza mtaala wetu kwa wakati na sehemu inayobaki ni ya mwanafunzi yeye mwenyewe kujitahidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi kama Serikali mkakati wetu ni kuhakikisha kwamba tunakwenda kutengeneza facilities za kuwezesha wanafunzi wetu kufanya masomo yao vizuri, ahsante sana.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuwaendeleza vijana wanaomaliza kidato cha nne na kupata daraja la nne au sifuri?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri haoni kwamba mtihani wa mwisho wa Kidato cha Nne mwanafunzi anapofanya wakati mwingine anaweza akawa amechanganyikiwa: Kwa nini sasa Wizara isiangalie matokeo yake ya nyuma ijumlishe na yale ya mwisho ili tuweze kumuhukumu kuendelea na maisha yake ya baadaye?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mtihani wetu wa mwisho wa Form Four siyo una-contribute au unaosababisha kuwa na matokeo ya mwisho. Mtihani wetu wa mwisho wa Form Four una maeneo mawili; asilimia 30 inakuwa kwenye maendeleo yake ya elimu, tunaita continuous assessment. Kwa hiyo, asilimia 30 ya zile alama (marks) zinatoka kwenye maendeleo yake yale ambayo ameyafanya kwa kipindi chote cha miaka minne; na asilimia 70 ndiyo ambayo inazingatiwa au inakuwa contributed na ule mtihani wake wa mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, iwapo amefanya vizuri kwenye maendeleo yake kutoka Form One mpaka Form Four, ile asilimia 30 ina maana itambeba na ule mtihani wa mwisho unachangia kwenye asilimia 70 tu ya mitihani yake. Kwa hiyo, hilo kama Serikali tumeshalizingatia na ndivyo inavyofanyika mpaka hivi sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuwaendeleza vijana wanaomaliza kidato cha nne na kupata daraja la nne au sifuri?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL C. MAKAMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru Serikali kwa kunipatia majibu kwenye swali hili la msingi, lakini nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa kutokana na uwekezaji mkubwa wa Serikali kwenye maeneo mbalimbali ya nchi hii kujenga Shule za Kata, kunakopelekea watoto wengi kumaliza Kidato cha Nne kwa alama hizo za Daraja la Nne au Sifuri na kwa vyuo hivyo vinavyotajwa na Serikali ni taasisi za Umma ambavyo vimejengwa kwa malengo ya kutoa elimu hizo kwa vijana wetu:-

Je, Serikali haioni sasa ipo haja ya kuwapangia moja kwa moja kwenye vyuo hivyo badala ya wao kuamua wenyewe?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tubebe ushauri wa Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu utaratibu huu sasa haupo wa kuwapangia moja kwa moja wale waliopata division four na zero au wale waliofeli darasa la saba. Kwa vile umetoa ushauri huo, acha tuuchukue kama Serikali twende tukaufanyie kazi, tufanye tathmini ya kina kama iwapo jambo hili linawezekana, basi tutaliingiza kwenye mipango yetu kama Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kuwaendeleza vijana wanaomaliza kidato cha nne na kupata daraja la nne au sifuri?

Supplementary Question 4

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ili mwanafunzi afikie kupata division zero au four ni pamoja na ufatiiaji hafifu wa masomo yake. Wazazi wanatakiwa wahudhurie mikutano ya shule wanapoitwa nakadhalika: Ni lini sasa Serikali italeta Muswada hapa Bungeni kuhakikisha kwamba tunatunga sheria ya wazazi kufatilia masomo ya watoto wao mashuleni? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la elimu ni suala ambalo linahusu pande karibu tatu; upande wa kwanza ni wanafunzi yeye mwenyewe, upande wa pili ni wa wazazi kama Mheshimiwa Mbunge alivyoshauri na upande wa tatu ni wa walimu au Serikali kwa ujumla. Kwa vile amezungumza hapa suala la kuleta Muswada Bungeni wa kuangalia namna gani tunaweza kuwabana wazazi ili waweze kufuatilia maendeleo ya watoto wao katika elimu, naomba tuubebe ushauri huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo tunafahamu kwamba katika shule zetu kunakuwa na Kamati mbalimbali za kufuatilia maendeleo ya shule pamoja na wanafunzi kwa ujumla. Kwa hiyo, nadhani Kamati zile sasa zinatekeleza wajibu huu, lakini kwa vile ni wazo au ushauri ambao ameutoa, acha tuuchukue kama Serikali twende tukafanye tathmini, halafu kama tukiona kama kuna umuhimu wa kuleta Muswada huo, tuweze kuleta hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.