Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Afya katika Kijiji cha Mikuwa Kata ya Mnanje Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niipongeze Serikali kwa jitihada kubwa ilizozifanya kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wananchi hawa wa Kata ya Mnanje, Wilayani Nanyumbu, wanapata ukombozi kwa kupata hii consent ambayo itaweza kupunguza pakubwa sana adha na changamoto katika Kata hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize swali maswali mawili ya nyongeza. Je, Serikali iko tayari kufanya jitihada za haraka kuleta hizi Milioni 250 ili kukamilisha ujenzi huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali itakuwa tayari kuleta watumishi wa kutosha ikiwa ni pamoja na vifaatiba ili kituo hiki kiweze kuanza kufanyakazi haraka na kwa wakati? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Boniphace Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamhakikishia tu kwamba hizi fedha Milioni 250, kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha huu Kata zote, maeneo yote ambayo tulipeleka fedha nusu, yatakuwa yamefikiwa ikiwemo katika Jimbo la Nanyumbu la Mheshimiwa Mhata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, mara baada ya kukamilika moja ya lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba tunanunua vifaatiba pamoja na kupeleka watumishi katika vituo vyote ambavyo Serikali imeanzisha, ahsante. (Makofi)

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Afya katika Kijiji cha Mikuwa Kata ya Mnanje Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 2

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Waziri Mkuu alipotembelea Kata ya Jangalu kwenye Kijiji cha Itolwa aliahidi kujengwa kituo cha afya. Naomba kujua ni lini sasa kituo hicho kitajengwa maana sasa ni miaka minne, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malengo ya Serikali kwanza ilikuwa ni kuhakikisha tunamaliza ujenzi katika Tarafa zote, lakini lengo la pili, ni kuhakikisha zile Kata ambazo hazifikiwa na zenyewe tunazijengea vituo vya afya. Kwa hiyo, hayo ndiyo malengo ya Serikali. Tatu, ahadi zote za Viongozi ambazo zimetolewa ziko katika mpango wetu tutahakikisha kabisa kwamba zinafikiwa ikiwemo katika Jimbo la Chemba, ahsante. (Makofi)

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Afya katika Kijiji cha Mikuwa Kata ya Mnanje Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 3

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa kupata nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri aweke kumbukumbu sawa ni Jimbo la Nanyumbu, naona maelekezo yako mengi yanazungumza Jimbo la Nanyamba, ni Jimbo la Nanyumbu, liko Mkoani Mtwara na Jimbo la Nanyamba pia liko Mkoani Mtwara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la nyongeza kumekuwa na ucheleweshaji wa fedha hasa kwenye hii miradi ambayo wananchi wanaiibua. Sasa katika Jimbo langu nina maboma zaidi ya Kumi ambayo mpaka sasa hivi hayajapata fedha.

Je, Serikali ina kauli gani juu yama boma hayo? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya lengo la Serikali ambalo hata kwenye bajeti tumepitisha, kila mwaka tumekuwa tukitenga fedha kwa ajili ya umaliziaji wa maboma ambayo yameanzishwa huko chini na wananchi pamoja na Serikali zetu kule chini. Kwa hiyo, tumekuwa tukitenga labda kwa kiwango fulani. Sasa hatuwezi kuyamaliza yote kwa wakati mmoja ila kwa wakati. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Mhata kwamba hata katika Jimbo la Nanyumbu, tutafanya hivyo katika mwaka wa fedha unaokuja kuongeza baadhi ya maboma ili tuhakikishe yanakamilika yote kwa wakati.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Afya katika Kijiji cha Mikuwa Kata ya Mnanje Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Serikali inajenga hospitali pale Ukerewe ambayo ikikamilika itakuwa na hadhi ya Mkoa na ikikamilika itakuwa inahudumia cases kubwa za rufaa. Sasa nataka kuiuliza Serikali haioni umuhimu sasa kuimarisha kituo cha afya cha Nakatungulu ambacho kitasaidia kuhudumia wagonjwa magonjwa ya kawaida na kikikamilika kitahudumia Kata zaidi ya Sita kwenye eneo la Mjini pale?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Mkundi, Mbunge wa Jimbo la Ukerewe kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tumekuwa tukiboresha vituo vya afya ambavyo vimekuwa na idadi kubwa ya watu na zile ambazo zinahudumia Kata nyingi ikiwemo katika hii Kata ya Nakatundu ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha. Kwa hiyo, bado iko katika mipango yetu na sisi tutaendelea kuziboresha kuhakikisha tunapeleka huduma za afya karibu na watu.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga Kituo cha Afya katika Kijiji cha Mikuwa Kata ya Mnanje Wilayani Nanyumbu?

Supplementary Question 5

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kufahamu ni lini Serikali itatujengea kituo cha afya katika Kata ya Vwawa ili kupunguza msongamano katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya kwanza ilikuwa ni kuhakikisha kwamba Tarafa zote zinapata vituo vya afya, hilo eneo ambalo analianisha ndiyo Makao Makuu ya Mkoa ambako tunayo hospitali ya Mkoa ambayo tumeipandisha hadhi kutoka hospitali ya Wilaya. Kwa hiyo, baada ya kumaliza hizo process zote ambazo tunazo sasa hivi, maana yake ndiyo tutafuatia hiyo hatua ambayo Mheshimiwa Mbunge anaainisha, ahsante. (Makofi)