Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Shule ya Sekondari Kalenga iliyopo Kata ya Ulanda kuwa ya kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 1

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru Serikali kwa majibu mazuri, ingawa shule hii ya Kalenga tayari imeshatimizi vigezo. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Kata nyingine ya Sekondari ya Isimila ambayo ina Kidato cha Tano na Kidato cha Sita, hii ina wasichana na wavulana. Mwaka 1999 aliyekuwa Rais wakati huo Mheshimiwa Hayati Mkapa alipita pale na akaahidi kujenga ukuta ili kuwalinda wanafunzi pale lakini mpaka leo haujakamilika.

Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunafahamu kule Marekani wameanzisha kitu kina Ben Carson Reading Clubs, huyu mwana sayansi Ben Carson alipata maarifa yake kwa kusoma kwenye maktaba.

Je, Serikali ni lini sasa itajenga Maktaba kwenye shule za Kata zote katika Jimbo la Kalenga.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ambayo ilitolewa ya ujenzi wa ukuta katika shule ya sekondari Isimila bado ipo na sisi niseme tu kwamba katika mipango yetu tumeiweka, kikubwa ambacho tunatafuta sasa hivi kwa sababu tuna mipango mingi sana ya kutafuta fedha, tutakapopata fedha kwa ajili ya kujenga maana yake tutaanza haraka iwezekanavyo. Lengo la Serikali kwa sasa ni kuhakikisha shule zote nchini zinapata maktaba zikiwemo hizo za Kalenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kikubwa tu ambacho tunabanwa sasa hivi ni bajeti lakini tunaendelea kutafuta fedha na ninaamini chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan tunaweza tukalifikia hili kama tulivyofanikiwa kwenye madarasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)