Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Ifumbo, Chunya?

Supplementary Question 1

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini sisi tunapenda kujua kwamba Serikali mradi huu wa maji wa Skimu ya Kata ya Ifumbo ulianza toka mwaka 2006 ni mradi wa muda mrefu na umetumia fedha nyingi sana za Serikali na kila siku Serikali imesema itakuwa inatenga fedha.

Je, ni lini sasa Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mradi huu uweze kuanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mto Lupa unaopita kwenye kata nyingi pamoja na vijiji vingi una maeneo mazuri sana yanayofaa kwa kilimo cha umwangiliaji.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kutuma wataalamu wake waweze kulitembelea hili bonde na baadaye waweze kuweka kwenye mpango na baadaye skimu iweze kujengwa kwenye Kata ya Mto Lupa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Rukwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatambua kwamba mradi huu ulikuwa ni wa muda mrefu na iko kazi ambayo inapaswa kufanyika ikiwemo ya ukarabati wa mfereji mkuu tumebakiza mita 750, lakini na mifereji ya shambani. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu ya umuhimu wa mradi huu tutaangalia pia vyanzo vingine vya fedha kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Umwagiliaji ili tuweze kukamilisha maeneo machache yaliyobaki ili wananchi waweze kutumia eneo hilo kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji hasa hekta 141 ambazo zimebaki.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la kuhusu kuwatuma wataalam, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba ndani ya wiki hii watendaji wa Tume ya Umwagiliaji nchini watakwenda kuangalia eneo hilo ili pia waje watushauri namna ya kuweza ya kuweza kutekeleza skimu hiyo. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Ifumbo, Chunya?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nina swali moja la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa umwagiliaji wa Bonde la Mto Ruichi uliopo Kigoma Mjini ili wanawake na wananchi wa Jimbo la Kigoma Mjini waweze kufaidika na kilimo cha kisasa? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zainab Katimba, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Ruichi hivi sasa tumeshapata no objection kutoka Kuwait Fund na utaanza utekelezaji wake mwaka huu wa fedha 2022/2023.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Ifumbo, Chunya?

Supplementary Question 3

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa skimu za umwagiliaji za Udimaa, Ngaiti na Chikuyu za Wilaya ya Manyoni ni chakavu sana, jambo hili limepelekea shughuli za kilimo cha mpunga kusimama.

Je, ni lini Serikali itakarabati skimu hizo ili shughuli za kilimo ziendelee? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aysharose Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Singida kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wabunge wote ni mashahidi na wameona kazi kubwa ambayo Mheshimiwa Rais ameifanya na dhamira njema ya kuongeza bajeti ya kilimo hasa kwenye eneo la umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge yakwamba timu yetu inaendelea kupita na kuyapitia maeneo mbalimbali ili kuweza kufahamu status ya miradi hii ya umwagiliaji. Lengo letu ni kuhakikisha miradi yote inafanya kazi. Halikadhalika kwa Singida pia kwa maeneo ambayo ameyataja nimuondoe hofu, tutakwenda kuyapitia na kuweza kuyafanyia kazi katika mwaka huu ujao wa fedha. (Makofi)

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Ifumbo, Chunya?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; Bonde la Mto Songwe lina eneo la kilometa za mraba 3,500 kwa ajili ya umwagiliaji.

Je, ni lini Serikali sasa itaanza kutekeleza mradi huo ambao unahusisha ujenzi wa dam pale kwenye Bonde la Mto Songwe?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Jumbe, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ukiangalia katika bajeti yetu ambayo tumeiwasilisha jedwali la kwanza yako mabonde 23 ambayo tunakwenda kuyafanyia upembuzi yakinifu na usanifu kwa ajili ya kuanza utekelezaji wake likiwemo Bonde la Mto Songwe. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ni sehemu ya mipango ya Serikali na tumedhamiria mabonde yote kuweza kuyafikia. (Makofi)