Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi watakaoathirika na ujenzi wa barabara ya Mwandiga – Manyovu Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; kumekuwa na malalamiko kwa wananchi kadha wa kadha ambayo bado wanaonesha namna gani ambavyo hawakupata stahiki hizo.

Ninaomba kujua ni lini Mheshimiwa Waziri utatenga muda ukawasikilize wananchi wale ili uweze kupata ufumbuzi wa malalamiko hayo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Assa Nelson Makanika, Mbunge wa Kigoma Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nipo tayari kwenda kuwasikiliza wananchi, lakini pia nitaomba tukubaliane naye mara baada ya Bunge hili muda sahihi na maeneo ambayo atataka Mheshimiwa Mbunge twende tukawasilize wananchi hawa ili tuweze kutatua hii changamoto ya fidia ambayo ni ya muda mrefu sana. Ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi watakaoathirika na ujenzi wa barabara ya Mwandiga – Manyovu Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, barabara ya Machine Tools kwenda Kialia Machame Girls ilijengwa mwaka 1930 kwa sheria ya mkoloni, lakini mwaka 2004 wananchi waliwekewa alama ya “X” nyumba zao wakarudia tena mwaka 2007.

Swali langu, je, ni lini Serikali italipa fidia wananchi ambao waliwekewa alama ya “X”?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, niwajibu na jukumu la Serikali kabla ya kuanza ujenzi wowote wa barabara kuhakikisha kwamba inalipa fidia; na kwa kuwa suala hili ni la muda mrefu mwaka 2004 - 2007 tunaongelea miaka kama 18 hivi. Kwa hiyo, nitamuomba Mheshimiwa Mbunge na nitoe agizo kwa Watendaji wa Wizara kutafuta documents zinazohusu barabara hii ili tuweze kukubaliana na Mheshimiwa Mbunge pia tuweze kwenda eneo hilo la barabara aliyoainisha kuongea na wananchi tuone tatizo ni nini ambapo mpaka sasa hivi hawajalipwa fidia hiyo. Ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi watakaoathirika na ujenzi wa barabara ya Mwandiga – Manyovu Mkoani Kigoma?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, wananchi waliokuwa pembeni ya barabara inayotoka Kongowe mpaka Kokoto wamefanyiwa uthamini zaidi ya miaka mitatu sasa.

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi hao ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Chaurembo, Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wananchi wa Mbagala ambao wamewekewa alama ya kupisha eneo hili la mradi huu kwamba kabla ya kuanza ujenzi Serikali itahakikisha inawalipa fidia yao. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha kwanza kuanza kwa ujenzi na kuwalipa hao wananchi fidia yao. Ahsante.