Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR aliuliza:- Je Serikali ina mpango gani wa kupitia upya fedha za Mfuko wa Vichocheo vya Maendeleo ya Majimbo na kuziongeza fedha kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili nyongeza. Kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majawabu yake haya mazuri.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza ningeomba tu kuuliza katika asilimia hizi alizozotaja karibu majimbo mengi ya Zanzibar tayari yameongezwa ukubwa wa eneo na kwa maana hiyo idadi ya watu pia imeongezeka, lakini hata ile hali ya uchumi ya wananchi kwenye majimbo hayo pia hayako vizuri.

Je, Serikali haioni sasa ndio muda muafaka wa kupitia upya vigezo hivi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili ni ushauri tu kwamba kiongezwe kifungu cha kuangalia gharama ya matumizi ya hizi fedha kwenye maeneo husika kwa sababu sisi kwa kule Zanzibar kama hizi fedha zinatumika kwenye miradi labda ya shule au madarasa vifaa vya ujenzi viko juu sana katika manunuzi yake. Kwa hiyo tungeomba kigezo hiki pia kiongezwe. Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la ndugu yangu Mohamed Suleiman Omar kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kweli majimbo mengi sasa hivi idadi ya watu imeongezeka na hili si kwa upande wa Zanzibar peke yake isipokuwa kwa nchi nzima na ndio maana mwaka huu kuna umuhimu mkubwa sana. Katika sensa yetu ya watu na makazi, ni vyema watu wakajitokeza tukapata idadi halisi ya wananchi katika maeneo husika, hata projection zozote za masuala ya miradi ya maendeleo iweze kuakisi uhalisia wa watu. Kwa hiyo jambo hilo ni jambo la msingi sana, ni imani yangu kubwa baada ya sensa yam waka huu tutapata takwimu halisi ya kila eneo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo ndio maana pale Naibu Waziri hapa alizungumza katika bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha tumeona ongezeko hili sasa limeongezeka kutoka shilingi bilioni 11 kwa majimbo yote mpaka shilingi bilioni 15.99, hay ani mafanikio makubwa na tuna kila sababu kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa utashi wake wa kuona majimbo haya lazima yaongezewe fedha.

Katika suala lingine la kuangalia au utaratibu mwingine wa kuboresha hili ni jukumu letu kama Serikali na hasa kuangalia masuala ya mipaka na mambo mengine. Naomba nikuahidi Mheshimiwa Mbunge na kama unavyofahamu kwamba jukumu langu kubwa hata nikija kule Zanzibar kwa kuchechua issue mbalimbali za kuhusu maeneo ya Zanzibar ambayo mimi nimepewa jukumu la kulisimamia, lengo letu ni kwamba wananchi wanaotarajia katika Mfuko wa Jimbo waweze kunufaika katika miradi ile inayogusa katika maeneo ya majimbo yao, ahsante sana.

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR aliuliza:- Je Serikali ina mpango gani wa kupitia upya fedha za Mfuko wa Vichocheo vya Maendeleo ya Majimbo na kuziongeza fedha kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, masuala mazima ya Mfuko wa Jimbo kwa wananchi wetu ni katika nia ya kuongeza maendeleo na mipango mizima ya kuinua uchumi wa wananchi wetu. Lakini Mheshimiwa Waziri katika Wizara yako kama utakumbuka Novemba mwaka jana Mheshimiwa Rais alipokuwa Glasgow alihutubia nchi tajiri na akaziomba kuongeza ufadhili wa fedha kwa nchi maskini ili kuweza kusaidia masuala mbalimbali ya kulinda mazingira. Fedha hizi zimekuwa nyingi sana, zimetolewa nyingi sana, lakini mbona Wizara hii iko kimya kutoa idhibaki (accreditation) kwa taasisi za Serikali na zisizo za Serikali kwa sababu tunafahamu kwamba nchi hii ikipata pesa hizi maendeleo yatapatikana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru sana dada yangu Lucy Mayenga kwa ufatiliaji wake na kwa kweli katika mkutano uliofanyika mwezi Novemba mwaka jana kule Glasgow, Scottish; Mheshimiwa Rais alizungumza mambo makubwa sana. Naomba niwaambie Watanzania katika mkutano ule hii image ya Tanzania imekuwa kubwa sana kwa Rais wetu katika kushughulikia masuala mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo alilouliza halihusiani na Mfuko wa Jimbo isipokuwa kama Serikali katika masuala ya miradi ya maendeleo ndio maana pale ofisini kwetu sasa hivi tunafanya kazi kubwa ya uandishi wa miradi. Na mtakumbuka mwaka huu itakapofika tarehe 5 Juni tutazindua mpango mkakati wa kutekeleza maeneo mbalimbali ambao mpango huo ndani yake una jinsi gani tunafanya resource mobilization ya upatikanaji wa fedha kushughulikia changamoto za kimazingira katika maeneo mbalimbali ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Name

Haji Amour Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR aliuliza:- Je Serikali ina mpango gani wa kupitia upya fedha za Mfuko wa Vichocheo vya Maendeleo ya Majimbo na kuziongeza fedha kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 3

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi nina swali langu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kisheria wahusika wakuu wa mfuko wa jimbo kwa upande wa Bara na Wizara inayohusiana na masuala ya Serikali za Mitaa, lakini kwa upande wa Tanzania Zanzibar wasimamizi wakuu ni Wizara ya Muungano inayohusika na masuala ya Muungano.

Swali langu je, ni sababu zipi fedha za Mfuko wa Jimbo kupelekwa katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais zisizimamiwe kupitia Ofisi ya inayoshughulikia masuala ya Muungano? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naomba kujibu swali la kaka yangu; ni kwamba Wizara yetu ni Wizara ya Muungano, lakini katika masuala ya uratibu kwa upande wa Zanzibar ofisi inayohusiana na masuala ya uratibu yote ni Ofisi ya Makamu wa Pili na hata hivi asubuhi nilikuwa naongea na pacha wangu, ndugu yangu Hamza katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo. Kwa hiyo, jambo hili halina mashaka, isipokuwa ni kwamba jambo kubwa linahitajika ni jinsi gani tutafanya kama kulikuwa na changamoto mbalimbali ya utekelezaji wa miradi lengo letu sisi kubwa kuweza kuingilia.

Mheshimiwa Spika, ndio maana nishukuru sana hata hapa nyuma Bwana Abdulwakil pale nilienda mpaka jimboni kwake wakanieleza masuala mbalimbali ya changamoto na tukaanza kuyatatua. Na mimi niwashukuru sana Wabunge wa Zanzibar baada ya kuibua changamoto mbalimbali za fedha za Mfuko wa Jimbo sasa ninaamini japo kama inawezekana matatizo bado yapo lakini naamini sasa hivi angalau kidogo speed ya utekelezaji imebadilika sana ukilinganisha na miaka ya nyuma iliyopita. Kwa hiyo tunaamini kwamba suala la uratibu linaenda vizuri mpaka sasa.