Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati Shule za Msingi za zamani katika Wilaya za Ileje na Mbozi?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ningependa niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; tunafahamu katika shule zetu nyingi za msingi miundombinu muhimu kama maji na umeme haipo. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha miundombinu hii inapewa kipaumbele katika shule zetu hizi hususan katika Mkoa wangu wa Songwe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; natamani kufahamu, huko kwetu shule nyingi za msingi zimekuwa hazina vyoo, hususan kwa Mkoa wangu wa Songwe na hasa zaidi katika Wilaya yangu ya Momba? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba baadhi ya miundombinu ya maji pamoja na umeme ambayo tunayo ina changamoto kubwa. Moja ya Sera ya Serikali ni kuhakikisha sasa hivi kwenye taasisi zote hizo za kielimu zinapatiwa umeme pamoja na maji. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, hilo lipo katika mpango wa Serikali na ndio maana sasa hivi unaona katika usambazaji wa umeme wa REA, wamekuwa wakiwapa vipaumbele taasisi hizo ambazo nimeziainisha hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusiana na maeneo mengi kukosa vyoo hususan shule zetu, katika bajeti ya mwaka huu, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo. Miongoni mwa vyoo tutakavyojenga ni katika Mkoa wa Songwe ambao yeye Mheshimiwa Mbunge ni Mbunge ambaye tunawakilisha pamoja. Ahsante sana.

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati Shule za Msingi za zamani katika Wilaya za Ileje na Mbozi?

Supplementary Question 2

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi. Shule nyingi za Msingi za Mkoa wa Lindi ni za zamani, zimejengwa mwaka 1947 na zingine kabla ya hapo, ikiwepo ya Lionja, Ngunichile, Kivinje, Ntua na kwingineko. Je, Serikali ina mkakati gani katika shule hizo? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tecla, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu katika mpango ambao tathmini inafanyika ni pamoja na hizo shule ambazo ameziainisha katika Mkoa wa Lindi na tathmini yetu itakapokamilika tutaainisha maeneo yote kila mmoja ni wakati gani utatekelezeka. Kwa hiyo nimwondoe shaka kwenye hilo. Ahsante sana.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati Shule za Msingi za zamani katika Wilaya za Ileje na Mbozi?

Supplementary Question 3

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Jimbo la Tabora Mjini lenye kata 29 lina matatizo kama hayo, lina shule nyingi sana za msingi ambazo ni kongwe na wananchi wamekuwa wakifanya juhudi ya kuzikarabati kwa juhudi zao wenyewe. Je, ni lini hasa huo mpango utaanza huu wa kuzisaidia kukarabati hizi shule kongwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu umeanza mwezi Aprili mwaka huu na utakamilika mwezi Julai mwaka huu. Mara baada ya kukamilika, tunaanza utekelezaji. Nimhakikishie tu kwamba tuko ndani ya mwaka wa utekelezaji na tutafikia shule zote ikiwemo hizi ambazo yeye ameziainisha. Ahsante sana.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati Shule za Msingi za zamani katika Wilaya za Ileje na Mbozi?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Mbozi ni moja ya Wilaya inayoongoza kuwa na shule nyingi za msingi, shule 179, lakini kiasi cha fedha za miundombinu na ukarabati zinazotoka Serikali Kuu kuja Wilaya ya Mbozi ni kidogo sana ukilinganisha na idadi ya shule 179. Sasa kwa nini Serikali isiangalie Wilaya ya Mbozi kwa jicho la tatu na kuangalia idadi ya hizi shule nyingi za msingi na kuongeza kiasi cha fedha kwa ajili ya miundombinu na ukarabati kwa ajili ya shule hizi za msingi? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mwenisongole, Mbunge wa Jimbo la Mbozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba Jimbo la Mbozi lina shule nyingi na lina majengo mengi ambayo bado hayajakamilika. Nimhakikishie Mbunge tu kwamba moja ya vigezo ambavyo tutavitumia sasa hivi ni kuhakikisha yale maeneo yenye uhitaji mkubwa tunayapa kipaumbele ikiwemo Jimbo la Mbozi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.