Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, tuna barabara inayounganisha Mikoa ya Kagera na Geita kutokea Katoke – Buharamulo kwenda kwenye Bandari ya Nyamirembe, na tuliahidiwa kwamba ingeanza kufanyiwa ujenzi mwaka huu wa fedha. Sasa tunaelekea ni mwezi wa tano sasa hivi imebaki miezi miwili hatujaona mkandarasi site.

Ni lini sasa barabara hii itaanziwa ujenzi ili wananchi wale waweze kuanza kuitumia ikiwa katika kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Ezra Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, barabara ya Nyamirembe – Katoke inatoka kwenye Bandari ya Nyamirembe ambayo tayari imeshakamilishwa na lengo ni kuunganisha hii bandari na Biharamulo. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ipo kwenye mpango na imeshaombewa kibali ili iweze kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi, naomba kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni lini barabara ya kutoka Bukombe kuja Katoro yenye urefu wa kilometa 65 itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Maana ni siku nyingi iliahidiwa.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maganga, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja inatekelezwa kwa mradi wa Rais, na taratibu zipo zinaendelea kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Nduguti – Iguguno yenye urefu wa kilometa 42 inayopita Makao Makuu ya Wilaya ya Mkalama kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aysharose Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum - Mkoa wa Singida, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mattembe kwa kufuatilia miundombinu ya Mkoa wa Singida. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama ilivyo kwenye Ilani ya CCM barabara hii itaanza kufanyiwa usanifu wa kina na kukamilisha mwaka unaokuja wa fedha ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Masasi – Nachingwea yenye kilometa 45 upembuzi yakinifu na wa kina umefanyika zaidi ya miaka tisa iliyopita. Ni lini Serikali itaanza ujenzi sasa barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chinguile, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ambayo inaunganisha Wilaya ya Masasi na Wilaya ya Nachingwea, kwa maana ya Mikoa wa Mtwara na Lindi, ni muhimu sana. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii kama bajeti ambayo tunategemea kuiwasilisha wiki ijayo itapita, ipo kwenye mpango kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali iliahidi kufanya upembuzi yakinifu wa barabara ya milimani ya Mwembe – Mbaga – Mamba – Ndungu ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Je, barabara hii ya Mwembe – Mbaga ya milimani ni lini itatengewa fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakuwa shahidi barabara hii mimi tayari nimeshaitembelea na kuiona na kuona changamoto zake. Moja ya vitu ambavyo Serikali tunavifanya kwa nature ya barabara yake, tumemuagiza Meneja wa TANROADS hata kabla ya kuanza kufikiria kuijenga yote kwa kiwnago cha lami, aainishe maeneo yote korofi ambayo kipindi cha masika hayapitiki ili Serikali iweze kuyajenga na kuhakikisha kwamba mwaka wote barabara hii inapitika. Lakini taratibu zipo kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara yote aliyoitaja ya Mwamba – Miamba – Ndungu ili kufanya maandalizi kwa ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali ambayo yana dhamira njema ya kuunganisha Mikoa ya Singida na Mbeya kwa barabara ya kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa maelezo yake Mheshimiwa Naibu Waziri; ni lini sasa huyu mkandarasi atafika Itigi ili wananchi nao waanze kufurahia matunda mazuri ya nchi yao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mkoa wa Singida unaunganishwa na Mkoa wa Simiyu kwa barabara ya vumbi kupitia Daraja la Sibiti. Je, ni lini sasa na barabara hii nayo itaweza kuanza ujenzi wa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali inapokea pongezi za Mheshimiwa Mbunge kwa kuanza ujenzi wa barabara hii. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati nakuja hapa Bungeni tayari mkandarasi wako wanasainiana mkataba na mara baada ya kufanya kazi hii naamini mkandarasi ataanza kukusanya vifaa ili kuweza kwenda kuanza hii kazi. Kwa sababu baada ya kusaini mkataba kazi inayofuata ni mobilization na kuanza kazi.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili la kuunganisha Mkoa wa Singida na Simiyu; barabara hii aliyoitaja ambayo inapita Daraja la Sibiti tayari imeshakamilishwa kwa kufanyiwa usanifu wa kina. Daraja limeshajengwa; nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pia kwamba katika mwaka huu wa fedha tumeongeza kilometa za kujenga barabara za lami ambazo zinaingia kwenye Daraja la Sibiti mpaka kilometa 25. Na Serikali katika bajeti inayokuja nina hakika tutaanza kwa awamu kujenga vipande vya barabara za lami ili kuunganisha Mikoa ya Singida na Simiyu kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa barabara ya Makambako – Songea ni mbovu na nyembamba sana na hivi juzi imeleta ajali na watu tisa wamefariki.

Je, lini Serikali itatengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami yenye ubora kutoka Makambo mpaka Songea? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Njombe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa kwamba barabara ya Makambako – Njombe hadi Songea ni barabara ambayo kwa kweli imechoka, ni barabara ya zamani sana, barabara ya tangu miaka ya 1984. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii tayari usanifu ulishakamilika na World Bank wameshaonesha nia ya kuijenga barabara hii upya ikiwa ni pamoja na kuipanua kwenye viwango vya sasa na mradi huu utahusisha pia na kujenga barabara ya bypass katika Mji wa Songea. Ahsante.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Mkiwa – Itigi hadi Rungwa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Singida utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa ya swali la nyongeza.

Mchakato wa mkandarasi wa kujenga barabara ya Ntendo – Muze imechukua muda mrefu takribani miezi 11 mpaka sasa. Nataka kujua ni lini mkandarasi anaripoti site kuanza ujenzi wa lami katika barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deus Sangu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Ntendo – Muze – Kiliamatundu ina package mbili; mkandarasi tayari ameshasaini kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kilometa za awali na kilometa zingine zinazoongezeka zipo kwenye taratibu za manunuzi. Kwa hiyo, muda wowote nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge mkandarasi atakuwa site kwa ajili ya kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami. Ahsante.