Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:- Je, Mwaka 2021 – Januari, 2022 Sekta ya Mifugo imeuza nyama nje ya nchi kwa asilimia ngapi na upi mkakati wa kuimarisha Sekta hii?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali kuhusiana na eneo hili, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mkakati wa Serikali umejikita kwenye wafugaji wapya wanatoka vyuoni. Ni nini mpango wa kuwawezesha wafugaji hawa wa sasa ambao wengi wanafuga kienyeji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; upande wa nyama ya kuku kumekuwa na tatizo la vifaranga mara nyingi. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha vifaranga vinapatikana ndani vyenye ubora ambao nyama yake inaweza pia kuuzwa nje? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia tasnia hii ya nyama nchini kwa umakini mkubwa. Nimwondoe shaka tu kabisa kwamba mipango ya Serikali siyo kwa vijana wanaotoka vyuoni, ama vijana wa kisasa pekee, ni pamoja na wale ambao wamezoea kufuga kwa mifumo ya kiasili. Kwa hiyo, mipango yetu inajumuisha makundi yote mawili na tunaendelea kufanya hivyo ili kuhakikisha kwamba tunaboresha mbari za mifugo kwa wafugaji wote nchini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu upatikanaji wa vifaranga, ndiyo moja ya mikakati ambayo sisi kama Wizara ya Mifugo na Uvuvi tunayo sasa hivi kuhakikisha tunaongeza uzalishaji ili vifaranga vipatikane kwa wingi na tuwasaidie wafugaji wetu, hususan wa kuku, na mifugo mingine, ili tuweze kuuza nje ya nchi kwa wingi mkubwa, ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza:- Je, Mwaka 2021 – Januari, 2022 Sekta ya Mifugo imeuza nyama nje ya nchi kwa asilimia ngapi na upi mkakati wa kuimarisha Sekta hii?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba niulize Wizara, kwa nini katika jimbo zima hakuna josho la kuogeshea wanyama?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mikakati ambayo tunayo katika mwaka wa fedha unaokuja, 2023/2024, Halmashauri ya Tarime ni miongoni mwa halmashauri ambazo zitapata majosho katika yale majosho ambayo tuliyatangaza katika fedha ambazo tuliziweka katika mpango, shilingi bilioni 5.7.