Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, mchakato wa mradi wa kutoa maji Ziwa Tanganyika umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nimesikia majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ninazungumzia kata 97 za Mkoa wa Rukwa ambazo hazina maji kutoka Ziwa Tanganyika na hapa wanasema wamejiandaa kwa mwaka wa fedha kumwandaa mtaalam mshauri.

Je, ni lini utaratibu wa kumpata huyo mtaalam mshauri na process kuanza mpaka mradi kukamilika kuanza kutoa maji kwa Mkoa wa Rukwa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, mwaja jana kata tano za Jimbo la Nkasi Kaskazini, tulinunua maji ndoo moja shilingi 800 mpaka 1,000.

Je, mna mkakati gani wa dharula wa kuweza kupeleka maji kwenye hizo kata wakati tunasubiri mradi mkubwa wa Ziwa Tanganyika ambao ndio suluhisho la jambo hili?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Aida Khenani, amefuatilia hili suala kwa muda mrefu na sisi kama Wizara tunakupongeza na hatutakuangusha na hatutakuwa kikwazo. Hizi Kata zote tutakuja kuhakikisha zinapata maji safi na salama. Lakini kwenye hizi kata tano za swali lako la pili, mkakati wa Wizara kwenye maeneo ya aina hii ni kutumia vyanzo vya maji rafiki vilivyokaribu, ikibidi kuchimba visima. Na kwa sababu tayari tuna magari basi tutachimba na kuweza kujenga vichotea maji na kuwasambazia wananchi ili kupunguza adha ya maji.