Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali italipa fidia kwa maeneo ya Kahe/Chekereni na Njiapanda yaliyochukuliwa na TANROADS mwaka 2013?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili licha ya majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali inaweza ikanihakikishia kwamba wananchi wa Uchira, ambao nao walipisha ujenzi wa upanuzi wa barabara hii inayotoka Arusha – Moshi kwenda Holili, je, nao watalipwa chini ya mchakato huu ulioanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, lini sasa barabara hii itaendelezwa toka pale ilipoishia Tengeru, eneo la Arusha kuja Moshi, Himo mpaka Holili?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikiri kwamba Mheshimiwa Dkt. Kimei kwa kweli suala la malipo ya fidia kwa hawa wananchi limekuwa ni suala ambalo kila tunapokutana na kuja ofiini analifwatilia, lakini tumelitolea majawabu na kwamba sasa tunakamilisha.

Mheshimiwa Spika, swali lake kuhusu wananchi ambao pia watapisha ujenzi, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa tulifanya tathmini siku za nyuma, tutarudia ku-review zile tathmini ili ziendane na muda wa sasa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Tengeru kuja huku Holili; JICA walishakubali, tumelijibu mara kadhaa, tutajenga hiyo barabara kwa kusaidiana na wenzetu wa Japan, ahsante.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: - Je, lini Serikali italipa fidia kwa maeneo ya Kahe/Chekereni na Njiapanda yaliyochukuliwa na TANROADS mwaka 2013?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Wananchi wa Jimbo la Nyang’hwale wanapenda kujua upembuzi yakinifu kuhusu barabara yao kutoka Kahama – Nyang’hwale mpaka Busisi, Sengerema utakamilika lini? Leo takribani miaka mwili tunaulizia jambo hili hatupati majibu, naomba majibu ya Serikali.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyang’hwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wiki iliyopita nilijibu pia hili swali. Hii barabara inahusisha mikoa takribani mitatu; Shinyanga, Geita na Mwanza. Upande wa Mwanza wanafanya Mkoa wa Mwanza, lakini kwa upande wa Shinyanga na Geita wanaosimamia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ni TANROADS Makao Makuu.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba walishakamilisha taratibu zote za kumpata Mhandisi Mshauri. Kwa hiyo, kazi inategemewa kuanza kwa sababu ni utekelezaji wa bajeti hii na wataendelea pia katika mwaka ujao wa fedha kuhakikisha kwamba wanakamilisha kuunganisha hiyo mikoa mitatu kupitia hiyo barabara aliyoitaja, ahsante.