Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mtwango?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, tangu Serikali ya Awamu ya Sita iingie madarakani Jimbo la Mufindi Kusini haikujengewa kituo cha afya hata kimoja, wakati maeneo mengine yamepata fursa hiyo. Wananchi wa Mufindi Kusini wana uhitaji mkubwa.

Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya cha Mtwango?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kwenda kujenga kituo cha afya Mtwango. Kwa hatua za mwanzo naomba nimuelekeze Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa kutuma timu kwenye eneo la Mtwango na kufanya tathmini na kuona mahitaji ambayo yako katika Kata ile, baada ya kufanya tathmini hiyo aiwasilishe Ofisi ya Rais – TAMISEMI Ili tuweze kuona ni namna gani tunapeleka fedha.

Mheshimiwa Spika, nimtoe mashaka Mheshimiwa Kihenzile Serikali hii ya Awamu ya Sita imeweka kipaumbele cha kujenga vituo vya afya kwenye maeneo yote ya kimkakati nchini ikiwemo kule Kata ya Mtwango Jimboni kwake.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mtwango?

Supplementary Question 2

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya upanuzi wa Kituo cha Afya cha Nyambiti ambapo imekuwa ikiahidi kila mara tunapouliza?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itapeleka fedha katika kituo hiki cha afya alichokitaja Mheshimiwa Kasalali Mageni kule Jimboni Sumve kadri ya uapatikanaji wa fedha, lakini tutatuma timu iweze kuangalia pia ukubwa wa eneo lililopo pia na majengo ambayo yanahitaji kufanyiwa upanuzi halafu tuweze kupata taarifa kamili na kutafuta fedha hizo.

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mtwango?

Supplementary Question 3

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, Kata ya Mapinga katika Jimbo la Bagamoyo katika sensa ya mwaka huu ina watu 42,000 na haina kituo cha afya.

Je, Serikali ina mpango gani kujenga kituo cha afya katika kata hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutatuma timu katika Kata ya Mapinga kule Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kuweza kufanya tathmini na kuona kama vigezo vimefikiwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya, halafu tutatafuta fedha kwa ajili ya kujenga kituo hicho cha afya.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mtwango?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa Kata ya Didia ni Kata ya kimkakati na ina idadi kubwa sana ya watu ukizingatia kwamba ni maarufu kwa zao la mpunga.

Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali hii ya Awamu ya Sita kuhakikisha inajenga vituo vya afya kwenye maeneo yote ya kimkakati nchini, ikiwemo Kata hii aliyoitaja Dkt. Christina Mnzava, tutafanya tathmini na kuona mahitaji yanayohitajika pale na kisha kuiweka kwenye mipango yetu ya kutafuta fedha. (Makofi)