Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni wanafunzi wangapi wamerejea shuleni tangu waraka wa kuwaruhusu utolewe?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza nataka kujua hao wanafunzi 1,907 waliorejea shuleni ni asilimia ngapi ya wanafunzi wote ambao walikatisha masomo na walipaswa warejee shuleni?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, nataka kujua kuna haja gani ya kuwaacha watoto nyumbani kwa kipindi cha miezi takribani minane tangu wafanye mtihani wa form four mpaka akajiunge na form five, pale pana muda mrefu; kuna sababu gani ya kuacha huo muda kwa sababu kutoka na matokeo ya sensa inaonesha drop out pia zinatokea hapo kwa kiasi kikubwa kwa sababu watoto wanakaa nyumbani muda mrefu, kwa nini muda ule usipunguzwe?

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili kama ulivyosema swali la kwanza linahusu takwimu. Naomba Mheshimiwa Mbunge aridhie baada ya kipindi cha maswali hapa Bungeni au baada ya Bunge tuweze kukutana kuweza kukokotoa hii percentage.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili anataka kufahamu mkakati wa Serikali juu ya kupunguza muda wa wanafunzi kusubiri kujiunga na kidato cha tano pamoja na vyuo vingine.

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna kipindi cha zaidi ya miezi saba baada ya wanafunzi kufanya mtihani wa kidato cha nne ili waweze kujiunga aidha na kidato cha tano au na vyuo vingine vya kati.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi hiki tunafanya mambo kadhaa ndio maana muda unakuwa mrefu, baada ya mithani kufanyika mwezi wa 11 zoezi la ukusanyaji wa zile script ambazo zimetumika kujibia mitihani huwaga zinakusanywa, lakini baada ya hapo tunakwenda kwenye zoezi la usahihishaji, tukimaliza usahihishaji tunakwenda kwenye zoezi sasa la uteuzi wa wanafunzi, lakini baadae hufanya maandalizi kwa ajili ya wanafunzi hawa sasa kuwapokea kwenye vituo vyetu vya shule mbalimbali. Kwa hiyo, shughuli ambazo zinafanywa katika kipindi hicho ni hizo.

Mheshimiwa Spika, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge Serikali imejidhatiti na kujipanga kwa dhati kuhakikisha kwamba tunapunguza muda huu ambapo sasa tumeanza utaratibu wa kufanya e-Marking kwenda kidato cha nne, tulikuwa tumeanza na darasa la saba kwa mithani ya darasa la saba, lakini sasa tunakwenda na hii mithani ya darasa la nne, tumeanzisha mfumo wa e-Marking ambao utapunguza muda wa usahihishaji, lakini eneo la pili katika upanganji vilevile tumeanzisha mfumo ambao unajulikana kama Management Information System ambao nao vilevile utapunguza muda wa upangaji au uteuzi ule wa wanafunzi kujiunga katika maeneo mbalimbali.

Kwa hiyo, tunapokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge wa kupunguza muda huo ili tuweze kuufanyia kazi sawasawa. Ninakushukuru sana.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni wanafunzi wangapi wamerejea shuleni tangu waraka wa kuwaruhusu utolewe?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Kwanza kabisa niipongeze Serikali kwa kuona watoto wengi wamerudi mashuleni, lakini mimi swali langu nilitaka kuuliza; je, Serikali inatoa elimu ya makuzi na malezi kwa hawa watoto ili hili tatizo lisiweze kujitokeza tena katika watoto wengine? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatoa elimu hiyo ya makuzi na malezi, lakini nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge katika rasimu ya mitaala pamoja na sera ambayo tunaendelea nayo hivi sasa, maoni ya wadau mbalimbali yameonesha kwamba kuna uhitaji wa masomo haya ya makuzi na malezi. Kwa hiyo, katika mitaala ijayo mambo haya tunaweza kuyaona kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)