Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Je, lini ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani – Nalasi hadi Tunduru utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Barabara ya kutoka Ipogolo kwenda Kilolo imekuwa ikiendelea kutafutiwa mkandarasi kwa muda mrefu. Napenda kujua ni hatua gani zimefikiwa na ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza? Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Barabara ya kutoka Ilula hadi Kilolo ambayo kipindi cha mvua huwa inakuwa imeharibika na Mheshimiwa Naibu Waziri kwenye majibu yake aliahidi kwamba itafanyiwa matengenezo, hadi sasa kuna maeneo bado: je, ni lini matengenezo hayo yatafanywa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Ipogolo – Kilolo yenye urefu usiopungua kilometa 33 ipo kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami kwa Mradi wa Rise. Tunapoongea sasa hivi Mbunge atakuwa na wananchi wa Kilolo wanafahamu kwamba, iko kwenye hatua ya manunuzi kwa ajili ya kuanza kujengwa barabara yote kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya pili aliyoitaja ya Ilula – Kilolo ambayo anasema mara nyingi inaharibika, ni kweli, eneo hili lina mvua nyingi, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya kipindi hiki cha mvua kwisha wakandarasi wapo, watakuwa muda wote wanaingia site kwa ajili ya kuikarabati hii barabara kwa kiwango ambacho itapitika bila matatizo, ahsante.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:- Je, lini ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani – Nalasi hadi Tunduru utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara inayotoka Tabora Mjini kupitia Mwanza Road ambayo inapita Bwawa la Igome mpaka kwenda Mambari - Nzega, ni muda mrefu haina lami na imekuwa ikisuasua: Lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli alichosema Mheshimiwa Mbunge wa Tabora. Nataka tu nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ipo kwenye ilani na tumeitengea fedha kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami, ahsante.