Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:- Je, lini zoezi la kufikisha umeme katika vitongoji, vijiji na mitaa ambayo haina umeme litakamilika Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lipo tatizo la umeme kukatika-katika hali inayosababisha vifaa vya umeme vinavyotumiwa na wananchi kuharibika.

Nini mkakati wa jumla wa Serikali kuhakikisha kwamba tatizo hili linaisha? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuja Wilayani Kakonko kwa ajili ya kueleza mazuri sana haya ya Serikali ambayo Serikali inaendelea kuyafanya? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Aloyce Kamamba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunakiri kwamba bado kuna maeneo yanayo tatizo la kukatika umeme na maeneo mengine kukatika ni kwingi, maeneo mengine ni kudogo, maeneo mengine tumepunguza kwa sehemu kubwa. Eneo analolisema linayo line ya siku nyingi ya kilometa zaidi ya 280 inayohudumia maeneo ya Kakonko, Buhigwe, Kasulu na Kibondo ambayo sasa imeunganishwa na line ya Gridi ya Taifa inayotokea Nyakanazi kwenda mpaka maeneo hayo yenye kilometa takribani 25.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti hii ambayo tunamaliza tumefunga kifaa kinachoitwa Auto Voltage Regulator ambacho kinaongeza nguvu ya umeme unaosafiri kwa muda mrefu ili angalau umeme uweze kufika mwingi kwa wadau mbalimbali. Katika bajeti inayokuja tumetenga pesa kwa ajili ya kwenda kuirekebisha na kuifanyia marekebisho makubwa hii line ikiwa ni pamoja na kubadilisha miti iliyochakaa, kubadilisha vikombe, lakini pia kubadilisha maeneo kidogo ya waya ambayo yamekuwa yakisababisha umeme kukatika kwenye maeneo haya.

Kwa hiyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kipindi kinachokuja cha mwaka wa fedha unaokuja katika kipindi kifupi ataona mabadiliko ya kurekebisha hii line ili iache kuwa inaathirika sana na matatizo ambayo yamekuwa yakitokea.

Mheshimiwa Spika, lakini katika eneo la pili, mimi niko tayari kwenda pamoja na yeye kuwaambia wananchi mipango mizuri kabisa ya Serikali, lakini pia na kusisistiza wao kushirikiana na Serikali katika kulinda miundombinu ambayo inapeleka umeme katika maeneo hayo, nakushukuru.

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:- Je, lini zoezi la kufikisha umeme katika vitongoji, vijiji na mitaa ambayo haina umeme litakamilika Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 2

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, ahsante, Mkoa wa Simiyu una jumla ya vitongoji 2,649 lakini vitongoji 1,713 havijafikiwa na umeme; je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vitongoji hivyo? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu wa vitongoji vyote 36,101 vya Tanzania Bara ambavyo havina umeme, na tayari mradi umetengenezwa tunaouita kwa kifupi HEP – Hamlet Electrification Project na tunatarajia mwaka wa fedha wa 2024/2025 tutaanza kuutekeleza na utaigharimu Serikali jumla ya kama shilingi trilioni 6.7.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuanzia katika mwaka wa fedha unaokuja Mkoa wa Simiyu, lakini kwenye majimbo yote mbalimbali yatapata vitongoji angalau 15 kwa kila jimbo. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Lucy kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Bariadi anakotokea washirikiane ku-identify vile vitongoji 15 vya kuanzia ili kupunguza changamoto, lakini katika ule mwaka mwingine tutaanza sasa kupeleka umeme katika vitongoji vyote ambavyo vinahusika.

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:- Je, lini zoezi la kufikisha umeme katika vitongoji, vijiji na mitaa ambayo haina umeme litakamilika Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 3

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, hii bajeti tuliyopitisha ya juzi ni kama mlishauriwa kuangalia ukubwa wa majimbo, siyo? Maana jimbo lenye kata nne kwa mfano, linafanana na lenye kata 36, lenye kata 39, hapo itakuwaje hapo wote wanapewa 15 vijiji na mitaa ama? Maana mlituahidi, sasa hili ni jibu unatoa leo, mnaenda kuangalia na ukubwa wa majimbo au ukubwa wa majimbo utakuja 2024/2025?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa bajeti tuliyokuwanayo sasa na kwa uhalisia uliokuwepo tumeona kipindi hiki cha kuanzia iwe ni vitongoji 15 kwa kila jimbo kwa sababu ni mwaka wa fedha mmoja, lakini katika mwaka wa fedha 2024/2025 hivi vitongoji 36,101 vyote tunatarajia kuvipatia fedha. Kwa hiyo, kipindi hicho sasa tutaanza na wale wenye mahitaji makubwa zaidi tukielekea kwenye mahitaji madogo zaidi. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:- Je, lini zoezi la kufikisha umeme katika vitongoji, vijiji na mitaa ambayo haina umeme litakamilika Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 4

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi, mimi leo nauliza je, ni lini sasa mtatupa jibu la uhakika la kutokukatika-katika umeme kwenye Jimbo letu la Temeke? Kwa sababu, mwaka 2021 hapa mlituambia mwezi wa Disemba umeme utakuwa sawasawa, mwaka 2022 mwezi Aprili utakuwa sawasawa, sasa ni mwaka 2023, je, ni lini? Tunaomba jibu la uhakika umeme kutokukatika-katika Temeke.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilave, Mbunge wa Temeke kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sababu za kukatika umeme kwenye maeneo mbalimbali zinatofautiana. Wako ambao umeme unakatika kwa sababu miundombinu yao imepita kwenye maeneo ya mapori na inasongwa sana na miti. Wako wenye maeneo mengine umeme unakatika sana kwa sababu wako kwenye maeneo yenye radi na mvua kali kwa hiyo, zile radi zinaathiri vile vifaa.

Mheshimiwa Spika, yako maeneo mengine kama ya mjini ambako miundombinu imezidiwa na matumizi ya wananchi, lakini pia yako mambo mengine shughuli za kibinadamu za kugonga nguzo kwa magari na vitu kama hivyo vinavyosababisha matatizo hayo yatokee.

Nimuahidi Mheshimiwa Kilave kwamba kwenye mradi wetu wa Gridi Imara kwanza tunaongeza uwezo wa mitambo yetu wa kupeleka umeme kwenye maeneo mbalimbali, na yeye ni shahidi kwamba kwenye maeneo ya Temeke tumeanza kupitisha miundombinu chini kwa maana ya underground ili tupunguze zile habari za malori na magari mengine kugonga zile nguzo.

Mheshimiwa Spika, sasa mradi huu wa Gridi Imara pamoja na miradi mingine ambayo tunayo ambayo tayari umeshaona inatekelezwa tunatarajia itakapokamilika katika kipindi cha mwaka mmoja au miwili ijayo maeneo mengi sana matatizo ya kukatika kwa umeme yatakuwa yamekwisha, lakini yapo matatizo mengine madogo madogo ya transfoma imezidiwa kwa sababu wakazi wameongezeka kama maeneo ya Kariakoo na vitu kama hivyo, tunavifanyia kazi kwa kadri vinavyotokea. Tunaomba tuendelee kushirikiana kupeana taarifa pale changamoto zinapotokea ili tuweze kuzifanyia kazi.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:- Je, lini zoezi la kufikisha umeme katika vitongoji, vijiji na mitaa ambayo haina umeme litakamilika Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 5

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi, Mkoa wa Katavi kwa ujumla una shida kubwa ya umeme kwa ujumla kwa sababu majenereta yaliyopo yameshindwa kuhimili idadi ya watu wanaotumia umeme. Serikali ina mpango gani wa dharura wa kupeleka jenereta litakaloenda ku-support umeme kwenye Mkoa wa Katavi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali katika mpango wa muda mrefu tunajenga sasa line ya kutoka Tabora – Ipole – Inyonga mpaka Mpanda Mjini kwa ajili ya kuhakikisha kwamba gridi imeufikia Mkoa wa Katavi, lakini katika njia za muda mfupi kama alivyouliza naomba baada ya hapa tutashauriana naye ili tuone tatizo ni kubwa kiasi gani na tuone ni wapi tunakoweza kupata mashine ya dharura ya kwenda kuongeza nguvu katika Mkoa wetu wa Katavi ili kipindi ambacho tunakamilisha upelekaji wa gridi basi wananchi waendelee kupata huduma ya umeme.