Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Nduguti kwa kuwa ujenzi wake umesimama kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, kituo hiki kilikuwa na plan ya kuwa Kituo A na kilishajengwa msingi kwa ajili ya ghorofa na ghorofa hilo lingekuwa na nyumba juu kwa ajili ya OCD. Sasa kwa sababu wamebadilisha na kuwa Kituo B, Serikali sasa ina mpango gani wa kepeleka fedha kwa ajili ya kujenga nyumba pembeni kwa sababu, sasa nyumba haitakuwepo tena juu?

Swali la pili, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari la Polisi kwa sababu tuna shida kubwa ya magari katika Halmashauri ya Mkalama? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu nyumba kwa ajili ya Askari au Mkuu wa Kituo ni kweli kwamba, awali ilikuwa kiwe Daraja A, lakini Sera ya Jeshi la Polisi inatambua Kituo cha Polisi Daraja A ni kituo kikubwa akinachostahili kujengwa kwenye ngazi ya Mkoa kwa maana ya kuwa chini ya Regional Police Commander (RPC), lakini hivi vinavyotokea ngazi ya Wilaya vinapaswa viwe Daraja B. Kwa hivyo, nyumba ile itatengwa katika bajeti ya mwaka 2024/2025 kutoka kwenye mfuko wetu wa tuzo na tozo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu gari la Polisi, juzi nilijibu hapa kwamba, tumetenga bilioni 15 kwa ajili ya ununuzi wa magari ya Polisi, magari haya yatakapopatikana, Wilaya ya Mkalama ni moja ya Wilaya itakayopelekewa gari na pikipiki kuwezesha shughuli za ulinzi na usalama wa raia. Nashukuru.

Name

Maryam Omar Said

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Pandani

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Nduguti kwa kuwa ujenzi wake umesimama kwa muda mrefu?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM OMAR SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na ufinyu na uchakavu wa ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, Mkoa wa Kaskazini Pemba. Je, ni lini Serikali itaanzisha ujenzi mpya kwa ajili ya ofisi hizi katika Mkoa huu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao mpango wa kujenga ofisi zote za Makao Makuu ya Polisi ngazi ya Mkoa. Kwa hiyo, tumeanza na Kusini Pemba, hatua itakayofuata ni Kaskazini Pemba ili Mikoa yote iweze kupata vituo vya Polisi vyenye ngazi ya Mkoa kwa maana ya Daraja A. Kwa hiyo, uwe na subira katika miaka miwili ijayo kituo hicho pia kitakuwa kimejengwa.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Nduguti kwa kuwa ujenzi wake umesimama kwa muda mrefu?

Supplementary Question 3

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, toka mwaka 2015 nilikuwa nikiomba tujengewe Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Kilindi. Naomba commitment ya Serikali juu ya ujenzi wa kituo hicho cha Polisi. Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa Kigua kwa uhakika kabisa kwamba, ni kipaumbele cha Wizara kupitia Jeshi la Polisi kwamba, Wilaya zote ambazo hazina vituo vya Polisi zinajengewa vituo vya Polisi. Nikupe assurance Mheshimiwa tutaangalia kwenye mpango wetu namna gani tunaweza tuka-fast track kutokana na majukumu muhimu ambayo Lindi inakabiliana nayo kwa maana ya uhalifu, mifugo, na kadhalika ili waweze kuwa na kituo cha polisi kumwezesha OCD kutimiza majukumu yake vizuri. Nakushukuru sana Mheshimiwa.