Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi; ni lini Serikali itaiongezea nguvu minara ya TTCL iliyoko katika Kata ya Maguliwa, Jimbo la Kalenga, Kata ya Wasa na minara ya Airtel ambayo iko Kata ya Ulanda?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama iifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuelewa kuwa kuna haja ya kuongeza nguvu katika minara kadhaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa tuna zaidi ya minara 800 ambayo inahitaji kuongezewa nguvu. Serikali imeanza na awamu ya kwanza ya kuongeza minara 408 na mpaka sasa kwenye mradi wetu wa Tanzania ya Kidigitali ni minara 302 inakwenda kuingizwa katika utekelezaji na kuhakikisha kwamba minara hiyo inapata nguvu ya kutosha na kupata huduma za internet.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimuombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo wakati Serikali inatafuta fedha ili tuhakikishe kwamba Tanzania yetu yote inakuwa ya kidigitali.

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; sasa licha ya Serikali kutoa namba ya kuwaripoti matapeli wa mitandaoni, je, Serikali ina mpango gani wa kuona sasa waathirika wanapata mrejesho badala ya kutegemea majibu ya automatic yale mifumo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ntara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimpongeze kwa swali zuri ambalo linatarajia kutoa elimu kwa watu wote. Kwanza kabisa, tuna namba 15040 ambapo ukikutanaa na namba za kitapeli basi unaweza ukatuma ujumbe na ujumbe huu utafika TCRA, baada ya hapo TCRA wataendelea kuufanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nipokee ushauri wa Mheshimiwa Mbunge wa kuona ni namna gani baada ya tatizo kufanyiwa kazi basi mtoa malalamiko aweze kupatiwa mrejesho.

Mheshimiwa Spika, tutalifanyia kazi, lakini vilevile napenda kuwaomba watanzania pale ambapo wanapigiwa simu na mtu akajitambulisha kwamba natoka Vodacom, Tigo na kadhalika basi naomba sana wapokee namba ambayo ni huduma kwa wateja ambayo ni namba 100. Tofauti na namba hiyo basi tuelewe kwamba hao sio watumishi wa Vodacom, Tigo wala kampuni yoyote ya mawasiliano, ahsante sana. (Makofi)

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 3

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; Vijiji vya Nsumba na Mboga, Kata ya Semembela na Kijiji cha Idubula na Burunde, Kata ya Karitu vimekuwa vikiwekwa kwenye mpango wa kujengewa minara kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote lakini karibu miaka miwili sasa inapita na minara haijengwi.

Je, sasa Serikali inatoa kauli gani au commitment gani kwamba safari hii vijiji hivi vya Nsumba, Mboga, Idubula na Burunde vitajengewa minara ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zedi, Mbunge wa Bukene kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ina dhamira ya kuhakikisha kwamba utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi inaendelea kutekelezwa kwa kiwango kikubwa. Ni kweli kabisa nchi yetu ina vijiji zaidi ya 12,300; tunakwenda hatua kwa hatua na tayari tunapeleka minara 758, tumefanya tathimini katika vijiji 2,224 lakini vilevile tunakwenda kupeleka minara 600 kwa ajili ya huduma ya mawasiliano katika vijiji vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaamini kwamba katika awamu ijayo vijiji vya Idubula, Burunde pamoja na vijiji ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja tutaviweka katika hatua hizo za utekelezaji ili wananchi wa Bukene wapate huduma ya mawasiliano bila kuwa na changamoto yoyote.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa Wilaya ya Kilolo imekuwa na changamoto nyingi sana na katika Wilaya hiyo hiyo kuna Kata ya Mahenge, Ukwega, Lugalo na Ihimbo wananchi wanapata shida sana ya mawasiliano.

Je, ni lini sasa Serikali itaondoa changamoto hizo ili wananchi wa Kilolo waweze kupata mawasiliano ya uhakika?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge wa Iringa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Kilolo walileta maeneo takribani 12 ambayo yalikuwa na changamoto ya mawasiliano, lakini eneo la Ilambo, Itimbo, Lugalo, Udekwa, Ukwega tayari tumeweka minara ya mawasiliano na huduma zinaendela.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kata nyingine ambazo tumezipelekea fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo takribani shilingi bilioni 1.28 imekwishapelekwa kwa ajili ya kujenga minara nane katika Kata saba za Jimbo la Kilolo, nakushukuru sana.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 5

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, baadhi ya maeneo ya Kata za Rungemba, Bumilayinga na Isalavanu na Kata ya Sao Hill hazina mawasiliano ya uhakika.

Je, ni lini Serikali itafunga japo mnara mmoja kuzunguka maeneo hayo ili wananchi hawa wapate mawasiliano ya uhakika? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nipokee changamoto ya Mheshimiwa Chumi ili Serikali ikafanyie kazi na pale fedha zitakapopatikana tutafikisha huduma ya mawasiliano, ahsante sana.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 6

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; kwa kuwa kama wateja tumekuwa tunaripoti hao wanaotutapeli kwa makampuni ya simu, lakini hatupati mrejesho.

Nini kauli ya Serikali kwa Makampuni ya Simu ambayo hayatupi mrejesho wa namna gani wana-deal na matapeli hawa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitumie fursa hii katika Bunge lako tukufu kuwaelekeza TCRA wakae na watoa huduma wote ili waone njia iliyosahihi zaidi ya kuhakikisha kwamba malalamiko yanayofikishwa basi Watanzania wanastahili kupata mrejesho wa malalamiko yao ili iwe rahisi kuweza kupima utekelezaji unakwenda kwa kipimo gani kulingana na malamiko yanayotumwa na mrejesho unaokuja. Hivyo, namwelekeza Mkurugenzi Mkuu na timu yake yote walifanyie kazi na sisi kama Serikali tutaendelea kufuatilia kwa karibu sana, ahsante sana.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 7

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ni suala la kawaida kuona sehemu “A” ina mtandao mmoja na sehemu “B” haina mtandao mwingine kwa maana hapa kuna Tigo, hapa kuna Vodacom.

Sasa ningetaka kujua ni utafiti gani ambao umefanyika na kuonesha mnara mmoja hauwezi kutoa mawasiliano ya mtandao zaidi ya mmoja? Moja, tukifanikisha hilo tutaweza kupunguza gharama, lakini pia tutaweza kupunguza madhara yanayotokana na hiyo mitandao au minara kwenye maeneo ya watu.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kagera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nitakuwa nimemuelewa vizuri anaongelea co–location; kama anaongelea co-location tunafanya cost benefit analysis ya watoa huduma anapoona kwamba hapa atakwenda kupata faida na pale atakapoona kwamba hawezi kupata faida hatoweza kufika pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana sasa Bunge lako tukufu lilipitisha Sheria Na. 11 ya mwaka 2006 kwa kuanzisha Mfuko wa Mawasiliano kwa wote ili kuhakikisha kwamba Serikali inakwenda kutoa ruzuku na kufikisha huduma ya mawasiliano katika maeneo ambayo hayana mvuto wa kibishara ili Watanzania wote wapate huduma ya mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa upande mwingine napokea ushauri wake na sisi tutaendelea kufanya utafiti ili kuboresha zaidi huduma ya mawasiliano nchini.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 8

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naipongeza Serikali kwa kunipa kandarasi ya utengenezaji wa minara tisa katika Wilaya yangu ya Kishapu, lakini kuna kata ya Ngofila, Kata ya Bunambiu na Mwasubi haziko kwenye orodha hiyo ya vijiji ambavyo vitakwenda kupata huduma hizo. Nini tamko la Serikali katika maeneo haya kuhakikisha kwamba huduma hiyo inapatikana?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimshukuru kwa kuipongeza Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumpelekea minara tisa aliyoipata katika kipindi cha miaka miwili. Kwa hiyo, tunaamini kwamba hiyo ni hatua nzuri kabisa ambayo tunatakiwa kuendelea kuishukuru Serikali hii, lakini vilevile hatutakomea hapo na awamu zinazokuja tutajiridhisha na changamoto iliyopo katika kata ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja ili tuziingize katika utekelezaji. Aidha, kama ni kuongeza nguvu ama kupeleka mnara, wataalam wetu watuambia ili kuhakikisha kwamba Watanzania wanapata huduma ya mawasiliano. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 9

MHE. DKT, CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, je, Serikali itakuwa tayari kuweka wazi mkeka wa mgawanyo wa minara 758 na hiyo mingine 600 tuliyoahidiwa? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Kimei, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iko tayari.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Kata za Masisiwe, Udwekwa na Nyanzwa Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 10

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kumuuliza swali Mheshimiwa Naibu Waziri wa Habari, Mawasilano na Teknolojia ya Habari, unakumbuka mwaka 2021 ulifanya ziara kwenye Jimbo langu ukawaahidi wananchi wa Mbogwe minara mitano, lakini mpaka sasa hivi haujatimiza ahadi yako.

Je, ni lini unakwenda kutekeleza ahadi yako ambayo mimi na wewe tulifanya mkutano kule Mbogwe?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maganga, Mbunge wa Mbogwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa nilifanya ziara katika Wilaya na Jimbo la Mbogwe na Serikali iliahidi kufikisha huduma ya mawasiliano, na mwezi wa saba wakandarasi wataingia field kwa ajili ya kuanza utekelezaji mara moja, ahsante sana.