Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Kampuni ya BG-EXXON MOBIL, OPHIR na washiriki wenzao wako tayari kuanza ujenzi wa LNGPlant. (a) Je, ni nini kinachokwamisha kuanza kwa utekelezaji wa mpango huo? (b) Je, ni hatua gani za makusudi zinachukuliwa ili kuharakisha utekelezaji wa mradi huo?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutoa elimu kwa wakati wa Mtwara na Lindi ili wapate uelewa juu ya mradi huu?
Lakini pili, waweze kujiandaa kutumia fursa zitakazopatikana baada ya ujenzi wa kiwanda hiki? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini pili, maeneo ambayo yalianishwa na mradi huu ni mawili, eneo la kwanza ni kwa ajili ya ujenzi wa kile kiwanda cha LNG, eneo la pili ni industrial park kwa ajili ya viwanda vingine ambavyo vitajengwa hapo baadaye.
Sasa nataka nijue hatua iliyofikia katika kutwaa eneo hili ambalo litajegwa viwanda vingine yaani eneo la industrial park kwamba je, wananchi wameshafidiwa au bado hawajafidiwa hadi sasa? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, mradi wa LNG ni mardi mkubwa sana, na nipende tu kusema kwa niaba yako na kwa niaba ya Wabunge; kati ya miradi mikubwa ambayo Serikali tumeitekeleza ni pamoja na mradi huu utakapo kamilika. Mradi huu kwa nchi za Afrika, Tanzania itakuwa ni nchi ya tatu katika kutekeleza.
Mheshimiwa Spika, lakini kujibu swali la msingi ambalo Mheshimiwa Chikota anataka kujua ni hatua gani imefikiwa katika kutoa elimu kwa wananchi; hatua tatu zimeshafanyika hadi sasa.
Mheshimiwa Spika, hatua ya kwanza ilikuwa ni kuwapa ufahamu na utambuzi wa manufaa ya mradi huu kwa viongozi wa Mikoa ya Lindi pamoja na Mtwara ambao vikao vimefanyika na kikao cha mwisho kilifanyika jana pamoja na juzi.
Mheshimiwa Spika, lakini hatua ya pili kulingana na hilo TPDC pamoja na wakandarasi na wazabuni waliopewa kazi hii wameshaanza kutoa elimu katika Vijiji vinavyoambaa katika mradi huu. Vijiji ambavyo vimeshatoa elimu hadi sasa ni pamoja na Kijiji cha Likong‟o ambapo mradi utachukuliwa, eneo la Kikwetu pamoja na Kijiji cha Mtomkavu. Hayo ni maeneo ambayo elimu wananchi wameshapewa kwa ajili ya umuhimu wa mradi huo.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili, kwamba ni maeneo gani yamechukuliwa kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda hiki. Kwa niaba ya wananchi ni vizuri niwatangazie kwamba eneo lililochukuliwa na mradi huu kimsingi ni eneo kubwa sana, ni jumla ya ekari 20,000 zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa mradi huu, hata hivyo kwa awamu ya kwanza kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa LNG ni hekta 2,071 zitatumika.
Mheshimiwa Spika, na kwa niaba ya wananchi ni vizuri nikiwaeleza, mradi huu utakapokamilika utakuwa na manufaa mengi kwa sababu wawekezaji mbalimbali watatumia maeneo haya. Kwa mujibu wa swali la Mheshimiwa Chikota, nikushukuru sana Mheshimiwa Chikota kwa sababu mradi huu ni vizuri sana Watanzania tukauelewa. Tunapozungumza kujenga uchumi wa viwanda ni pamoja na viwanda vikubwa kama kiwanda hiki ambacho nimekieleza.
Mheshimiwa Spika, ahsante sana.