Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, lini Serikali itaboresha Kivuko cha Kinesi?

Supplementary Question 1

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Kivuko cha MV Musoma kilitolewa na Serikali na kivuko kilichopo hakikidhi mahitaji na kina changamoto nyingi sana, kinaweza kusababisha matatizo: Je, ni lini Serikali itarejesha Kivuko kile? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa miundombinu ya ujenzi kule Kinesi inahusisha maeneo waliyokuwa wanamiliki wananchi pale Kinesi: Je, lini Serikali itawalipa fidia wananchi wale ili waweze kupisha mradi huo? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Kivuko cha MV Musoma ambacho kilikuwa kinafanya kati ya Mwigobero na Kinesi kilihamishwa kwenda kutoa huduma katika Kivuko cha Kisorya na Rugezi kwa sababu ya ukubwa wake. Kivuko cha Totuu kilitolewa Chato kwenda Musoma kufanya kazi kwa sababu kituo kilichokuwa kinafanya kazi kati ya Nansio kwa maana ya Kisiwa cha Ukerewe na Kisorya kilikuwa kimeharibika na kilikuwa kinahitaji matengenezo makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachotaka kumwambia Mheshimiwa Mbunge ni kwamba Kivuko cha MV Ujenzi ambacho kinafanya kazi kati ya Rugezi na Kisorya tuko kwenye hatua za mwisho kabisa. Kilichokuwa kinafanyika ni kubadilisha engine, sasa tunapaka rangi. Tunaamini mwishoni mwa mwezi wa Saba, kivuko hicho kitakuwa kimekamilika ili MV Musoma iweze kurudi kwenda kufanya kazi kati ya Mwigobero na Kinesi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu matengenezo au ujenzi katika eneo la Kinesi, tayari tumeshafanya tathmini na tumeshaainisha wananchi watakaopisha ujenzi wa maegesho. Hivi tunavyoongea sasa hivi, taratibu za kuandaa majedwali ya kuwalipa zinaendelea ili mwakani tunapoanza tuweze kujenga maegesho upande wa Kinesi pamoja na miundombinu yake, ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, lini Serikali itaboresha Kivuko cha Kinesi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Wizara ya Ujenzi ilitenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vivuko vipya: Ni lini ujenzi huo wa vivuko vipya utaanza pale Kigamboni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika mwaka huu unaoendelea, Serikali ilitenga fedha za kujenga vivuko vingi, vikiwemo vya maziwa na vya pale Kigamboni alivyovisema Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tunategemea kujenga kivuko kimoja kikubwa, lakini pia kumetokea maombi kadhaa na Serikali inafanya tathmini kuona baada ya kupata uzoefu wa vivuko hivi vidogo vya Bakhresa, namna ambavyo tunaweza kufanya ni kujenga kivuko kibwa na pia kuwa na vivuko vidogo. Kwa hiyo, kinachoendelea sasa hivi, tuko kwenye taratibu za manunuzi kuhakikisha kwamba kile tulichokipanga tunakifanya pia katika mwaka huu, pamoja na kuongeza vivuko vidogo ambavyo tumeona vinakwenda kwa haraka sana kati ya Kigamboni na Kivukoni, ahsante.