Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:- Je, Serikali ina mchango gani katika kuboresha huduma za Hospitali ya KCMC ambayo inatoa huduma za afya kwa Kanda ya Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itatekeleza maombi ya kibali cha mabadiliko ya mishahara katika hospitali ya KCMC ambacho wameomba tangu mwaka 2011?

Swali la pili; kuna upungufu mkubwa wa wafanyakazi katika Hospitali hii, je, Serikali imejipanga vipi kuweza kutatua changamoto hiyo, ikizingatiwa hospitali hii ni ya Kanda?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyoshirikiana na Wabunge wa Mkoa wa Kilimanjaro na namna ambavyo anafanya kazi yake. Swali lake la kwanza kuhusu ni lini Serikali itafanya maombi yale ya kupandisha hadhi na kuongeza mishahara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu swali la kwanza la kuhusu Mbeya Mbeya pamoja na KCMC ni hospitali ambazo ziko kwenye mchakato ambao kuna mjadala kati ya Wizara ya Afya, Wizara ya Fedha na Utumishi kwa ajili ya kufikia kiwango hicho ambacho Mheshimiwa Mbunge unakitaja. Wiki hii tumepanga tufanye kikao na utumishi ili tuweze kuona ni namna gani tunaweza kujikwamua na kusaidia vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni suala la upungufu wa watumishi. Kama ambavyo nimesema kuna watumishi 905 ambao wanalipiwa na Serikali, lakini wao wenyewe wanalipa kwa mapato yao ya ndani zaidi ya watumishi 400. Maana yake ukiangalia wanao watumishi karibu 1,300 sasa huo upungufu labda tutaenda kuangalia upungufu umetokana na nini. Inawezekana huko nyuma kweli kulikuwa na upungufu unaoletwa na hospitali yetu ya Mawenzi ilikuwa haifanyi vizuri, sasa hospitali yetu ya Mawenzi sasa inafanya vizuri kwa hiyo, wagonjwa wengi watazuiliwa Mawenzi, wataenda wale wanaohitaji kwenda kwenye Hospitali ya Kanda kwa hiyo, huo upungufu unaweza usionekane. (Makofi)