Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, lini Serikali itatunga Sera ya Ugatuaji wa Madaraka na kutunga sheria ili kuzijengea uwezo Mamlaka za Serikali za Mtaa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu hayo ya Serikali ambayo yamenipa mashaka katika mawanda ya ushirikishwaji wa wadau, niseme tu kwamba, katika sehemu ambayo Serikali inatakiwa kuwa makini ni katika kutunga sera hii kwa sababu, ndiyo inakwenda kujibu Ibara ya 146 ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Swali la kwanza; Ni kwa kiwango gani wadau katika Mikoa, Wilaya na Halmashauri na kwa upekee wake Waheshimiwa Madiwani wameshirikishwa katika utungaji wa sera hii?

Swali la pili; Je, Serikali iko tayari kutoa commitment hapa Bungeni kwamba, katika mchakato huu kabla ya maamuzi sera hii ipitiwe na Wabunge, kama tulivyopitia Sera ya Elimu, kwa lengo la kutoa input zaidi na kuboresha utungaji wa sera hii?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Ally Kassinge, swali lake la kwanza anasema ana mashaka, nimtoe mashaka haya kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ina imani kubwa na Sera nzima ya D by D na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, chini ya uongozi wake Mheshimiwa Angellah Kairuki itaendelea kusimamia sera hii ya D by D ambayo ni ugatuaji wa madaraka kwenye Halmashauri. Halmashauri hizi ziweze kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi yao wenyewe kwa kushirikiana na wataalam ambao wanapelekwa na Serikali katika maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye Sali lake la pili ambalo anataka commitment, commitment kama nilivyosema hapo nikimjibu swali lake la nyongeza la kwamba, Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaamini katika D-by-D. Baada ya mwongozo huu kufanyiwa mapitio tutaileta kwenye Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ili nao waweze kupitishwa kwenye mwongozo ule ambao upo, lakini tutabaki katika D by D Mheshimiwa Mbunge na hatutatoka katika hilo kwa ajili ya kuwapa nguvu Waheshimiwa Madiwani kufanya maamuzi yao katika Halmashauri zao.