Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Ofisi za kisasa za Walimu katika kila shule nchini?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini je, haioni iko haja ya kufanya nguvu zaidi kwa ajili ya shule hizi za sekondari ambazo ni kongwe hasa katika Jimbo langu la Temeke, Shule ya Kibasila?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; je, Serikali haioni iko haja ya kuongeza pia nguvu katika shule ambazo zilianza kujenga ofisi hizi lakini mpaka sasa hazijaendelezwa mfano kwangu, shule inaitwa Ally Hassan Mwinyi ambayo ni jina kubwa sana. Je, ni lini sasa Serikali itaweza kumalizia ofisi hizo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dororth Kilave, Mbunge wa Temeke, kwanza kuhusu kuongeza jitihada ya Serikali kwa ajili ya kukarabati na kujenga shule hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge na wana-Temeke kwa ujumla kwamba, Serikali hivi karibuni imepeleka shilingi milioni 700 katika Shule ya Sekondari Kibasila kwa ajili ya ujenzi wa mabweni na madarasa, likiwemo jengo la utawala katika shule ile. Kwa hiyo, ni jitihada kubwa za Serikali hii ya Awamu ya Sita katika kuhakikisha inaboresha miundombinu ya shule za sekondari na shule za msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke na nchini kote.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali la pili kuhusu shule zilizoanza ujenzi wa majengo haya ya utawala zenyewe, ikiwemo shule ya Ali Hassan Mwinyi, nitakaa na Mheshimiwa Mbunge na kuona ni namna gani Serikali inaweka jitihada kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa jengo hili la utawala katika shule hii yenye jina la Rais wetu wa Awamu ya Pili, Mheshimiwa Dkt. Ali Hassan Mwinyi.