Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa mahitaji ya Walimu wa shule za msingi katika Jimbo la Babati Vijijini ni 1,956 na waliopo ni 1,226 na hivyo kuwa na upungufu wa Walimu 730. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha Walimu wanaopatikana katika shule za msingi? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishasema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali inaendelea kuweka kipaumbele cha kuajiri Walimu na hasa katika shule za msingi kuhakikisha inapeleka Walimu wa kutosha kwenye maeneo yenye upungufu ikiwemo kule Jimboni kwa Mheshimiwa Sillo. Katika hao 13,130 tutaangalia ni mgao kiasi gani ambao Mheshimiwa Sillo amepata kule katika Halmashauri yake na nitakaa naye kumpa hiyo orodha.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mkoa wa Tabora ni moja kati ya mikoa ambayo shule nyingi sana ziko katika maeneo ya vijijini na hazina Walimu wa kutosha. Je, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kupeleka Walimu maeneo hayo ili kunusuru elimu ya Mkoa wetu wa Tabora?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikitoa kipaumbele katika maeneo mbayo yana upungufu wa walimu ikiwemo Mkoa wa Tabora na ndio maana katika miaka ya fedha iliyopita ikiwemo wa 2021/2022, ukijumlisha wote Mkoa wa Tabora ulipokea Walimu 1,111 na kwa kutambua bado kuna upungufu huo, Serikali ndio maana ilitoa ajira 13,130 kwa kupitia kibali alichokitoa Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan. Kwa sababu Mheshimiwa Rais anapeleka fedha nyingi za ujenzi wa miundombinu ya madarasa naku – invest hela nyingi katika elimu hapa nchini, Serikali itaendelea kuweka kipaumbele cha kuajiri Walimu na ikiwemo katika Mkoa ule wa Tabora.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali itapeleka Walimu wa kike katika shule ya msingi iliyoko Nkasi inaitwa Shule ya Itete na Shule ya Kala?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, katika ajira hizi mpya 13,130 ambazo Serikali imetoa katika mwaka huu wa fedha tutaangalia na kuweka kipaumbele katika shule hizi alizozitaja za Itete na Kala kule Wilayani Nkasi.

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Katika Jimbo la Same Magharibi maeneo ya milimani hasa Kata za Msindo, Mshewa, Vudee, Tae, Suji, Chomi, Muhezi na Ruvu kuna shida kubwa sana ya Walimu na kwa sababu pengine mazingira magumu ya milima. Je, ni lini Serikali itapeleka Walimu wa kutosha katika kata hizo za milimani na kuwapatia motisha? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itapeleka Walimu katika mgao huu wa hawa 13,130, Wilaya ya Same nayo itapata Walimu hawa kwenda kufanya kazi kule na tutaendelea kuajiri kadri ya bajeti itakavyoruhusu kwa ajili ya kuweza kupeleka Walimu kwenye maeneo yote yenye upungufu hapa nchini, ikiwemo kule kwa Dkt. Mathayo, Wilayani Same.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 5

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Serikali imeboresha, imejenga shule nyingi za msingi na sekondari na kuna uhaba wa Walimu. Je, Serikali ina mpango gani wa kukidhi mahitaji ya Walimu ambao ni takribani Walimu 1,000 ni pungufu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali mipango yake ya kuhakikisha hakuna upungufu wa Walimu katika Wilaya ya Tanganyika na wilaya zingine hapa nchini, ndio maana imeendelea kuajiri na hivi karibuni ajira 13,130 zimetolewa za Walimu kwa ajili ya kwenda kuziba mapengo na uhitaji uliopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo kule Tanganyika.

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 6

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa majibu mazuri ya Wizara, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza; Serikali haioni kwamba kuna haja ya kuweka motisha kwa Walimu walioko vijijini, ili tuweze kupata Walimu wengi waweze kwenda kuajiriwa vijijini ili tuweze kuondokana na upungufu maeneo ya vijijini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; Serikali haioni kuna haja ya ajira hizi zinazotoka nyingi zielekezwe vijijini? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza aliyouliza Mheshimiwa Kainja. La kwanza hili la motisha kwa Walimu vijijini, tayari Serikali inalifanya hili kwa kupitia Wakurugenzi wa Halmashauri husika, kuna Halmashauri ambazo Walimu wanaporipoti kazini wamekuwa wakipatiwa magodoro na vifaa vingine vya kuweza kuwapa motisha kubaki katika maeneo yao ya kazi. Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kule imekuwa ikifanya hivyo na maeneo mengine nchini na tutaendelea kuona ni namna gani tunatoa motisha kwa Walimu hawa wanaoenda vijijini kadri ya upatikanaji wa fedha na uwezo wa Serikali na bajeti kuruhusu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, la haja ya ajira hizi hawa Walimu kwenda vijijini. Walimu hawa wanaajiriwa kutokana na upungufu uliopo kwenye maeneo husika hasa maeneo haya ya vijijini. Sasa naomba nitoe rai hapa kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ambao ndio waajiri wa Walimu hawa na wale wa Mkoani Tabora kule anakotoka Mheshimiwa Kainja vile vile, kuhakikisha kwamba hawa wanaopangiwa maeneo haya kwenda kufundisha wanabaki kule kwenye maeneo yale kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma. Kwa sababu Serikali ilifanya review ya maeneo yote yenye upungufu wa Walimu na ndiyo maana hawa wanaajiriwa kwenda kuziba mapengo yale yaliyokuwepo kwenye maeneo yale.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kila mmoja akiomba kuhama, ina maana mapengo yale yanazidi kuwepo. Vile vile nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote Serikali itaendelea kuajiri Walimu hawa kwa ajili ya kuziba mapengo haya na upungufu uliopo kadri ya bajeti itakavyoruhusu.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 7

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa fursa hii, kwa kuwa Wilaya ya Namtumbo ni wilaya ambayo iko pembezoni kabisa mwa nchi hii Kusini mwa Tanzania mpakani na Msumbiji na ina upungufu mkubwa wa Walimu katika shule zake za msingi. Je, Serikali inaweza ikatupa umuhimu kutugawia Walimu wa kutosha katika shule zetu zenye upungufu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua upungufu uliokuwepo katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo kule Jimboni kwa Mheshimiwa Kawawa na katika ajira hizi mpya 13,130, Wilaya ya Namtumbo nayo itapata mgao wa Walimu wapya kwa ajili ya kwenda kupunguza upungufu uliopo kule wilayani.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi hii. Kwa kuwa Halmashauri zote za Mkoa wa Shinyanga hasa vijijini zina upungufu mkubwa wa wafanyakazi. Je, ni nini kauli ya Serikali kutatua tatizo hili?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Dkt. Mnzava kwamba, Serikali itaendelea kutatua upungufu wa watumishi wa umma ikiwemo Walimu katika Mkoa wa Shinyanga na mikoa mingine hapa nchini kadri ya bajeti yake itakavyoruhusu na ndio maana katika bajeti ya 2022/2023 Serikali ilitenga ajira 21,000 kwa ajili ya Walimu na kada ya afya, kwa ajili ya kupunguza upungufu uliopo kote nchini ikiwemo kule Shinyanga.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 9

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na mgao huu wa Walimu 13,100 Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ziko shule zilionekana zina upungufu sana wa Walimu, lakini katika mgao huo hazikupata Mwalimu hata mmoja, ikiwemo Shule ya Msingi Litoho. Je, ni lini, sasa Serikali itapeleka Walimu kwenye Shule hii ya Msingi Litoho na shule nyingine za Halmashauri ya Mbinga?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu upungufu ambao ameuzungumzia Mheshimiwa Kapinga uliokuwepo kule Wilayani Mbinga, Serikali ndio maana imekasimu mamlaka kwa Makatibu Tawala wa Mikoa kufanya msawazo wa Walimu kuhakikisha shule mbalimbali zinapata Walimu kwa kutoa maeneo yenye Walimu wengi zaidi na kuwapeleka kwenye maeneo yenye uhitaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu, kumwelekeza Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma kuhakikisha kwamba anapeleka Walimu kwa kufanya msawazo ndani ya Mkoa wake katika shule alizozitaja Mheshimiwa Kapinga.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Shule za Msingi katika maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 10

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri amesema kwamba mwajiri wa Walimu hawa ni Mkurugenzi wa Halmashauri, lakini Mkurugenzi huyo wa Halmshauri amemnyima nafasi ya kukataa uhamisho wa mtumishi, jambo linalofanya watumishi wengi kuchukua namba tu kwenye hizi wilaya ambazo zipo pembezoni na kuondoka. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha Wakurugenzi wanakuwa na Mamlaka ya kuhamisha kulingana na wanavyoona nafasi inayopatikana?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kuchauka. Hili la kukataa uhamisho liko wazi, Waraka wa Katibu Mkuu Utumishi unaeleza wazi kwamba mtumishi wa umma anapoajiriwa atatumikia mwaka mmoja wa probation na baada ya mwaka ule anatakiwa kukaa katika kituo chake kipya cha kazi kwa muda usiopungua miaka miwili kabla ya kuomba uhamisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, namna utaratibu ulivyo ni lazima mtumishi anapoomba uhamisho katika barua yake ile awaweke pale KK, Mkuu wake wa Shule, amuweke Afisa Elimu wa Wilaya, amuweke muajiri wake ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri na wale wote wanatakiwa kuweka comment pale, kama wanaona kuna uhaba wa watumishi katika maeneo yao, katika barua ile wanavyoandika imepitishwa, aandike kwamba kuna uhaba na huyu nashauri asihame. Barua ile inapofika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, wataangalia na zile comment za mwajiri na kuzifanyia kazi na kuhakikisha kwamba Mwalimu yule au mtumishi yule hatoki katika maeneo yale ikiwemo kule Liwale. Kwa hiyo naomba Mkurugenzi wa Liwale afuate utaratibu.