Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kwa kutengeneza barabara zote mbovu katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Mji wa Kharumwa unazidi kupanuka na matengenezo yanafanywa ya mara kwa mara kwenye barabara zetu za mitaa pale Kharumwa, lakini zinaponyesha mvua barabara zile huwa zinaharibika kwa ajili ya ukosefu wa mitaro. Je, Wizara iko tayari kutenga fedha kwa ajili ya kujenga hiyo mitaro ili kunusuru uharibifu wa barabara hizo wakati wa mvua?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TARURA imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya maboresho ya Mji wa Kharumwa kule Wilayani Nyang’wale anakotoka Mheshimiwa Amar na tutaendelea kuangalia ni namna gani tunapeleka fedha ya kutosha kadri ya upatikanaji wake, kwa ajili ya kuboresha mazingira ya mji huu hasa ujenzi wa mitaro ambayo upo kule Wilayani Nyang’wale. Nimtoe shaka Mheshimiwa Mbunge, yeye ni shahidi vile vile kwamba TARURA imeongezewa fedha zaidi ya mara tatu ya ile iliyokuwepo mwaka wa fedha 2020/2021 na hii ni commitment kubwa ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Watanzania kwa kutenga fedha ya kutosha kwa TARURA kuhakikisha barabara nyingi zaidi zinatengenezwa.

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kwa kutengeneza barabara zote mbovu katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 2

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Serikali kupitia TARURA, Mkoa wa Simiyu iliahidi kujenga Daraja la Mto Sanjo linalounganisha Itilima na Meatu na Daraja la Mto Sanga linalounganisha Maswa na Meatu kwa muda mrefu. Je, ni lini Serikali itatimiza azma yake hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itatimiza azma ya kujenga madaraja haya katika mito hii miwili aliyoitaja Mheshimiwa Mpina, inayounganisha kati ya Wilaya ya Itilima na Wilaya ya Maswa, lakini kuna mingine ambayo ametaja pia ya Wilaya ya Meatu anakotoka yeye Mheshimiwa Mpina. Tutaangalia katika bajeti hii ambayo tunaenda kuitekeleza 2023/2024 na kuona ni kiasi gani kimetengwa na nitakaa na Mheshimiwa Mpina kuweza kuona tunaanza vipi kwa haraka kadri ya fedha iliyotengwa ya ujenzi wa madaraja haya mawili.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kwa kutengeneza barabara zote mbovu katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, majibu ya Serikali ni mazuri sana na Mkoa wa Simiyu umepewa fedha kwa ujumla kama walivyopewa Mikoa mingine. Namuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa umuhimu wa Mkoa wa Simiyu kwa sababu ya zao la pamba, kwa sababu kuna njia mbovu sana kwa mfano sasa hivi tunakwenda kusafirisha mazao ya pamba njia ni mbaya sana kutoka vijijini.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari sisi kwa kushirikiana na TARURA tulete hesabu ya kipekee kwa ajili ya kupambana na tatizo hili ili muweze kutujengea barabara mbovu katika Mkoa wa Simiyu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyongo la kuleta maombi ya kipekee; hivi sasa Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imeteua timu ya kufanya mapitio ya namna ya kutoa mgao wa fedha za barabara kwenye Halmashauri zetu kote nchini kwa kuangalia umuhimu wa maeneo, kuangalia masuala ya kilimo yaliyokuwepo hapo, upitwaji wa magari kwa wingi na kadhalika.

Kwa sasa TARURA ilirithi mfumo ambao ulikuwa katika Road Fund ya namna ya mgawanyo wa fedha hizi zinazopelekwa, lakini baada ya timu hii kumaliza itawasilisha taarifa yake kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI na baada ya kuwasilisha taarifa hiyo, watakaa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, pamoja na TARURA kuona ni namna gani sasa mgawanyo wa fedha utaendana kutokana na mazingira yaliyoko katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo kule Jimbo la Maswa anakotoka Mheshimiwa Nyongo.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kwa kutengeneza barabara zote mbovu katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 4

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara nyingi za ndani ya Mji wa Mugumu kule Wilayani Serengeti zina hali mbaya sana na haziwezi kupitika; je, ni lini sasa Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amsabi Mrimi la lini Serikali itaongeza ukarabati wa barabara zake katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti?

Mheshimiwa Naibu Spika, nilijulishe Bunge lako tukufu kwamba hivi tunavyoongea hivi sasa kuna barabara ambayo inazunguka Soko Kuu la Mji wa Mugumu ambayo inatengenezwa kwa kiwango cha lami kupitia Wakala wetu wa TARURA na tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha mazingira ya Mji wa Mugumu kwa sababu ndiyo Makao Makuu ya Wilaya ya Serengeti. Lakini vilevile kupitia Wilaya nzima ya Serengeti barabara za changarawe vilevile tutaendelea kuhakikisha fedha inatengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara zake na nyingine Mheshimiwa Mbunge Mrimi amekuwa akija kwa ajili ya kuzielezea na kusema barabara zipi ziweze kutengewa fedha kwa ajili ya kuzifungua.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kwa kutengeneza barabara zote mbovu katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 5

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Moja; kwa kuwa changamoto za barabara na za Mkoa wa Simiyu zimekuwa zikiongezeka siku hadi siku, barabara ni mbovu, wananchi wanashindwa kupita na kusafirisha mazao yao; je, Serikali ina mpango gani sasa wa muda mfupi kuhakikisha wanarekebisha barabara za Mkoa wa Simiyu zile ambazo zinachangamoto kubwa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa changamoto ya barabara za Mkoa wa Simiyu inafanana na zile za Mkoa wa Dar es Salaam. Mkoa wa Dar es Salaam umekuwa na changamoto kubwa ya barabara chakavu lakini na kukosa mitaro hali ambayo inasababisha wakati wa mvua shuhuli zote za kiuchumi kusimama katika Mkoa wa Dar es Salaam; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha wanajenga mitaro na kurekebisha ili sasa wakati wa nyakati za mvua magari yaweze kupita? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza la kwanza hili la mpango wa barabara za Mkoa wa Simiyu kama ambavyo nimeisha kwenye majibu yangu ya msingi, ukiangalia mwaka 2021 Serikali ilikuwa imetenga shilingi bilioni tano kwa Mkoa wa mzima wa Simiyu kwa ajili ya ukarabati wa barabara lakini kuonyesha ni namna gani Serikali inajali wananchi wa Mkoa wa Simiyu, inajali wananchi wake wa Tanzania iliiongezea fedha TARURA kutoka shilingi bilioni 226 na kwenda shilingi bilioni 776 zaidi ya mara tatu ya ile bajeti ya mwanzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ukiangalia Mkoa wa Simiyu peke yake kutoka shilingi bilioni tano kwenda shilingi bilioni 17 ambayo imetengwa kwa ajili ya mwaka wa fedha 2023/2024. Hivyo Serikali itaendelea kuweka kipaumbele cha kuhakikisha kwamba barabara zinatengenezwa kwa wakati ili ziweze kupitika na kuendelea kupunguza asilimia ya barabara mbovu kwa kuhakikisha TARURA inaendelea kuwekewa fedha kwa ajili ya matengenezo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la pili kuhusu Mkoa wa Dar es Salaam; wewe pia ni shahidi kwa sababu ni Mbunge wa Mkoa wa Dar es Salaam tayari hivi karibuni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Angellah Kairuki alikaa na Wabunge wote wa Mkoa wa Dar es Salaam na vilevile aliita Kamati ya Bunge ya TAMISEMI na kusaini mikataba kwa ajili ya kuanza Mradi wa DMDP II ambayo itakwenda barabara zote ambazo zinachangamoto, zilizosalia ambazo hazikuwepo kwenye DMDP I katika Mkoa wa Dar es Salaam ni zaidi ya shilingi bilioni 800 ambayo Serikali hii ya Mama Samia Suluhu Hassan imetenga kwa ajili ya kuhakikisha Mkoa wa Dar es Salaam unaboreka. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kwa kutengeneza barabara zote mbovu katika Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii. Sehemu kubwa ya Jimbo la Arumeru Mashariki liko kwenye miteremko ya Mlima Meru, kwa hiyo barabara zake kwa mwaka mzima zinakuwa ni mavumbi au mifereji wakati wa mvua. Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha kwa ajili ya kuzijenga kwa kiwango cha lami au tabaka gumu la namna nyingine kwa teknolojia nyingine yoyote? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo la barabara zake hizi za Arumeru Mashariki kwamba, Serikali imeweka commitment kubwa kwa kuiongezea fedha TARURA kuhakikisha barabara nyingi zaidi zinatengenezwa kwa kuwapa bajeti mara tatu ya ile ambayo Dkt. Samia Suluhu Hassan aliikuta mwaka 2021. Sasa tutakaa na Mheshimiwa Dkt. Pallangyo tutazidi kuangalia ni namna gani TARURA inaweza ika-fast track utengenezaji wa barabara hizi ambazio wananchi wa Arumeru Mashariki wanazihitaji.