Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiongeze kundi la wanaume kwa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Tarimba Abbas, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Serikali iko kwenye maboresho ya utoaji wa hizi asilimia 10; Serikali haioni ni wakati sahihii wa kufanya marekebisho ya sheria pia ili kuongeza kundi la wanaume kwenye utoaji wa mikopo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili; kwa kuzingatia mila, desturi na utamatudini wetu, jamii nyingi ya Tanzania mwanaume ni kiongozi wa familia; hauoni kwa kumuondoa mwanaume kwenye utoaji wa mkopo ni kufanya kumdumisha mwanaume lakini ni ubaguzi unaoondoa umoja wetu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Tarimba, ambayo yameulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Mafuwe la kwanza juu ya maboresho haya, kwa sasa kama ambovyo amesema mwenyewe Mheshimiwa Mbunge, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI ipo katika mapitio ya sera hii na sheria hii kwa ajili ya kuona ni namna gani inaweza kuboreshwa kuendana na wakati wa sasa na tayari kuna timu ambayo wajumbe wake wameshateuliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mheshimiwa Kairuki na imeishaanza kazi yake na pale itapomaliza kazi yake basi tutaleta kwenye Bunge hili kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI na baada ya hapo kuileta ndani ya Bunge hili kwa ajili ya kuweza kufanya marekebisho ya sheria hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la kuwa na wanaume ni namna gani wanaingizwa kwenye unufaikaji wa mikopo hii? Tayari timu hii itaangalia pia uwezokano wa hili lakini katika makundi haya wanaume wapo kwenye makundi ya vijana, wanaume wapo katika makundi ya walemavu lakini tutachukua ushauri wa Mheshimiwa Mafuwe na kuona ni namna gani nao tunaweza tukaangalia wanaingizwaje katika kupata au kunufaika na mikopo hii.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiongeze kundi la wanaume kwa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Serikali inaendelea na maboresho na VICOBA ni vikundia ambavyo wananchi ususani wanawake wa Kilimanjaro wameshamiri sana; ni kwa nini VICOBA visiusishwe sasa katika mikopo hii ya asilimia 10?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokuwa nikisema awali maboresho haya yanafanyika kwanza ni kutokana na maagizo aliyoyatoa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya kuangalia upya utoaji wa mikopo hii kwa vikundi. Kwa hiyo, naamini katika timu ambayo inafanya kazi watapitia pia hili la VICOBA kuona uwezekano au upi ni urahisi kuweza kuwafikia wananchi wengi zaidi.