Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itashughulikia kuboresha ujira wa madereva wa magari ya IT?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Serikali ndiyo msimamizi mkuu wa mwananchi wa kawaida, hauoni kwamba kuna haja sasa ya Serikali kutoa tamko kwa wamiliki wa magari haya ya IT kwa kuwa wao wanapoingia mikataba wanawadhulumu hawa madereva. Sasa Serikali itoe tamko kuhakikisha wanafuata kile ulichosema cha kima cha chini ili na wao wapate mikataba halali ya kuweza kuendesha magari hayo na kupata ujira unao stahiki badala ya kilometa 900 kulipwa shilingi 100,000? Swali la kwanza hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa utaratibu unaonesha deriva wa IT aruhusiwi kuwa na msaidizi, tukumbuke kwamba magari haya yanaenda kilomita nyingi sana kwa mfano toka Dar es salaam mpaka Tunduma ni zaidi ya kilometa 900 hakuna haja sasa ya Serikali kuruhusu madereva hawa wawe na wasaidizi ili wapunguze ajali? Kwa sababu mara nyingi magari yao yanadondoka njiani kwa uchovu wa madereva kwa kuwa mtu mmoja peke yake?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hebron Mwakagenda, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhusiana na suala la hawa madereva wa IT kuwasimamia na kuratibiwa na Serikali tayari tunayo Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, lakini pia tunayo sheria kwa makubaliano wanayoyafanya mara nyingi wanafanya makubaliano kwa njia ya mdomo. Tumekuwa tukishauri kwa wakati wote kwamba waingie makubaliano kwa maandishi na sababu ya msingi ni kwamba hizo siyo ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu utoaji wa gari ni wa mtu binafsi au kampuni labda anaagiza gari kutoka Japan linapopitia Bandari ya Dar es Salaam kuipeleka nje ya nchi. Kwa hiyo inakuwa ni kazi ya siku moja au ya wakati tu ambapo dereva atakuwa amefikisha gari hiyo kwenye eneo husika, lakini hata hivyo tumekuwa tukizingatia kwamba katika kipindi cha kufanya kazi hiyo azingatie sheria ambayo ya mkataba ambao ni Sura Namba 345 inayo elekeza maslahi ya watu kwanza wanaoingia kwenye mkataba maslahi, lakini pili kuangalia uzito wa kazi yenyewe husika na ikiongozwa na hili amri ya ajira ambayo ya mishahara hii ambayo tumeitoa ya kima cha chini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tutaendelea kusimami hivyo, lakini kwa wale ambao wanafanyakazi kwenye makampuni tumekuwa tukisisitiza wakati wote kuweza kuhakikisha wanakuwa na mikataba ya kazi ili kulinda haki hizo zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili amelieleza kuhusiana na hao madereva wa IT kwa nini hawarusiwi kuwa na msaidizi ndani ya gari? Kwenye hili nitalichukua kwa sababu linahusiana pia na Wizara ya Mambo ya Ndani ili kuhakikisha kweli hawa watu wanakuwa na usalama, lakini pia kuongeza usalama kwa watumiaji wa vyombo vya moto katika barabara. Kwa hiyo, talichukua kwa ajili na nanii nishukuru kwamba ni pendekezo zuri tutalizingatia, ahsante.