Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kibondo pamoja na nyumba za Askari Polisi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza kabisa naishukuru Serikali kwa majibu mazuri ambayo yameonesha matumaini kwa kuwa wameshafanya tathmini, lakini, je, Serikali haioni kwamba iko sababu ya kuharakisha ukarabati wa nyumba hizi ili kuboresha ufanisi wa askari angalau kwa kuanza na pesa kidogo mwaka huu, then mwaka kesho tumalizie? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, haja ya kufanya haraka ya kuharakisha upatikanaji wa hizi huduma ni jambo la msingi na sisi kama Wizara tutahakikisha kwamba tunakwenda kutafuta fedha kokote ziliko ilimradi tuhakikishe kwamba Vituo vya Polisi nchini kote ikiwemo Jimbo la Mheshimiwa Mbunge la Muhambwe vituo hivi vifike.

Mheshimiwa Spika, hii ni kwa sababu ya azma njema ya Mheshimiwa Rais ya kuhakikisha kwamba kwanza wananchi wote wanapata huduma za ulinzi na usalama, lakini pia kuhakikisha kwamba tunaboresha mazingira yawe mazuri zaidi kwa upande wa vyombo hasa Jeshi la Polisi ikiwemo magari na Vituo vya Polisi na nyumba za makazi, nakushukuru.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kibondo pamoja na nyumba za Askari Polisi?

Supplementary Question 2

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je ni lini Serikali sasa itamaliza nyumba za askari eneo la Barracks Kilwa Road ndani ya Jimbo la Temeke?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nataka nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba azma ya Serikali ni kuhakikisha kwamba Vituo vyote vya Polisi ikiwa vya Wilaya ikiwa vya Mikoa itahakikisha kwamba vinakamilika, lengo na madhumuni wananchi wajue sasa wapi wanakwenda kupeleka changamoto zao, kwa sababu tumegundua bado kuna baaadhi ya maeneo yakiwemo wilaya na maeneo mengine bado hayajapata Vituo vya Polisi. Kwa hiyo nimwambie tu Mheshimiwa kwamba tutahakikisha kwamba Kituo cha Polisi kinakuja na fedha zitakapopatikana, tutahakikisha kwamba tunampa kipaumbele kwa ajili ya kupata hicho Kituo cha Polisi.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kibondo pamoja na nyumba za Askari Polisi?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Uvinza?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, inatambua umuhimu wa uwepo wa Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Uvinza. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajitahidi. Kokote tutazitafuta fedha zilipo ili tuhakikishe kwamba tunapeleka Kituo cha Polisi katika Jimbo lake ili mradi wananchi waweze kupata huduma za ulinzi na usalama na mambo mengine ya kipolisi, nakushukuru.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kibondo pamoja na nyumba za Askari Polisi?

Supplementary Question 4

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Je ni lini Serikali itaweka bayana mpango mzima wa ukarabati au ujenzi wa Vituo vya Polisi pamoja na nyumba za kuishi kwa nchi nzima ili kuepuka kudaiwa huduma hii kila kukicha?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nataka nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeshaanza kufanya tathmini ya kuona namna ambavyo tunaweza tukauandaa huo mpango. Kwa hiyo nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajitahidi kadiri iwezekanavyo tuone namna ambavyo tunauhangaikia huo na kuweza kuanza kuufanyia kazi kama ambavyo Mheshimiwa ametaka. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati kwenye Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kibondo pamoja na nyumba za Askari Polisi?

Supplementary Question 5

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika Kijiji cha Mkundoo na Mkusinde kumekuwepo na matukio kadhaa yameripotiwa ya uhalifu. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi eneo hilo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumekuwa tukiripotiwa baadhi ya matukio ambayo mengi yao yamekuwa yakisababishwa na wananchi wenyewe kwa wenyewe, lakini nimwambie tu kwamba Serikali haijalala kwa maana kwamba ipo makini kuhakikisha kwamba tunapambana dhidi ya vitendo vyote vya uhalifu ikiwemo na kuhakikisha kwamba tunatafuta magari kwa ajili ya kufanya doria na ukaguzi wa mara kwa mara ikiwemo na kujenga Vituo vya Polisi kwa ajili ya wananchi ili kuweza kwenda kupeleka changamoto zao na kuweza kutatuliwa kwa haraka, nakushukuru. (Makofi)