Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Bwalo la Shule ya Sekondari Igwachanya Njombe?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, ni lini Serikali itakarabati na kujenga upya majengo ya shule chakavu Wilaya ya Njombe, Ludewa, Wanging’ombe na Makete ndani ya Mkoa wa Njombe?

Swali la pili, ni lini Serikali itatua tatizo la upungufu wa Walimu wa Sayansi ndani ya Mkoa wa Njombe? ahsante.(Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mgaya, swali lake la kwanza kuhusu ni lini Serikali itakarabati shule hizi kongwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Daktari Samia Suluhu Hassan ilikwisha karabati shule 89 hapa nchini, ambapo kule Mkoani Njombe kuna shule mbili ambazo zilipata fedha ya kukarabati ambayo ni shule ya Kivavi Sekondari iliyokuwepo Wilayani Makambako vilevile Njombe sekondari. Tunaendelea kuangalia ni namna gani tunaweza tukaendelea ukarabati wa shule kongwe ikiwemo zile zilizokuwepo Mkoani Njombe. Nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mheshimiwa Kairuki analishughulikia hili suala kuona ni namna gani atapata fedha ya ukarabati wa shule hizi kongwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la Walimu wa Sayansi. Hivi sasa Serikali ipo katika ukamilishaji wa mchakato wa kuajiri Walimu wa Sayansi na walimu kwa ujumla ambao ni 13,390 ambao wataanza kazi muda Serikali mrefu. Kwa hiyo, nikutoe shaka Mheshimiwa Neema Mgaya kwamba kule Mkoani Njombe nanyi mtapata mgao wa Walimu hawa ambao wanakuja. Mheshimiwa Neema amekuwa akilifatilia sana hili suala na nimwakikishie kwamba Serikali imekusikia na italifanyia kazi suala la upungufu wa walimu katika Mkoa wa Njombe. (Makofi)