Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Je, kwa nini Serikali inaajiri kwa kigezo cha mwaka wa kumaliza chuo na kupitia mafunzo ya jeshi?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, ni zaidi ya miaka mitano imepita tulikuwa hatuna ajira katika Taifa letu, tunaonaje kama tusibadilishe angalau utaratibu kwa sababu wale wa miaka mitano ambao hawajaajiriwa na mkawataka wa hivi karibu hatuoni kama tunawaacha nje kwenye mfumo wale ambao walimaliza kwa miaka hiyo mitano ya nyuma? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa JKT zamani ilikuwa ni mujibu wa sheria kila mwanafunzi akimaliza anaenda mwaka mmoja JKT lakini sasa hivi bajeti kwa kuwa ndogo wananchaguliwa wachache. Hatuoni kwamba tunawanyima nafasi wale wachache ambao hawajachaguliwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kumekuwa na gap hilo la miaka mitano kama alivyoeleza Mheshimiwa Mbunge, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pia kulihakikishia Bunge lako kwamba ziko jitihada za maksudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha kwamba gap hilo tunalitoa.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora kwa kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI tumekwishaanza kufanya jitihada hizo na unayoyaona yanayotokea sasa ikiwemo kuongezeka kwa matangazo ya nafasi za ajira ni moja kati ya hatua hizo zinazofanyika.

Mheshimiwa Spika, juu ya jambo la pili, kuhusu vijana ambao wameachwa katika kipindi hiki cha miaka mitano iliyopita ambao hawajajiunga na JKT, ambao Mheshimiwa Mwakagenda anasema ni group la wasomi. Nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge pia kulihakikishia Bunge lako kwamba Serikali katika utaratibu huo huo imeendelea kufanya juhudi za maksudi kuhakikisha kwamba gap hilo nalo tunalifunga ili vijana wengi wa Kitanzania waweze kupata fursa hiyo. Kwa kweli katika jambo hili nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kutoa vibali vingi sana vya ajira katika kipindi cha mwaka 2022/2023 ambapo vibali 20,000 vilitoka pia 2023/2024 ambapo vibali zaidi ya 30,000 navyo vimetolewa kwa ajira mbalimbali ikiwemo ikiwemo ajira hiyo ya vijana ambao wamekosa sifa za kuingia JKT.