Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, ni lini Muswada wa Ukomo wa Upelelezi wa Kesi utaletwa ili kupunguza msongamano wa kesi unaotokana na upelelezi kutokamilika?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu ya Serikali ni mazuri na imeonesha kwamba sheria ipo, lakini ukweli ni kwamba utekelezaji wa sheria hii umekuwa ni hafifu sana. Pia kama hivyo ndivyo, Watanzania wengi wamekuwa wakiathirika na utekelezaji huu hafifu wa hii sheria, kitu ambacho kinawafanya waathirike kisaikolojia, kijamii na hata kiuchumi. Vilevile wanapotoka na kuja mtaani baadaye watu hawa wanakua wamepoteza uelekeo sana lakini tunajua utekelezaji huu hafifu wa hii Sheria umeipa mzigo mkubwa sana Serikali kwa kuwahudumia watu ambao wanakaa muda mrefu rumande. Kitu ambacho tulivyofanya ziara mbalimbali tumeona kabisa kuna watuhumiwa wengi…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Neema, uliza swali.

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wananchi wengi wako gerezani kwa zaidi ya miaka 15. Swali la kwanza; je, Serikali ina mkakati gani wa kuwalipa fidia watuhumiwa wote waliokaa mahabusu muda mrefu na kushinda kesi hizo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, nataka kufahamu ni nini kauli ya Serikali katika kufuta kesi zote za watuhumiwa waliokaa zaidi ya miaka mitano mahabusu?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Naomba sasa nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Neema Gerald, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sio kweli kwamba haya tunayoongea hapa hayatekelezeki, ndio maana ukiangalia kwenye takwimu zetu za masijala za mahakama hadi jana tarehe 29/5/2023 mashauri ni 1,863 lakini backlogs ambazo hazijafanyiwa kazi ni asilimia nne tu. Hapa maana yake ni nini? Maana yake Mahakama imekuwa ikizisikiliza kesi hizi na zimekuwa zikihukumiwa na kuondoka na sasa katika mahakama zetu hakuna kesi ambayo mtuhumiwa yuko mahabusu mpaka sasa zaidi ya miaka mitano hajahudumiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumshukuru Mheshimiwa Rais, amekuwa akiboresha mahakama zetu, amekuwa akiteua Majaji, amekuwa akitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama Kuu na mwaka huu wa fedha tunakwenda kujenga Mahakama za Mikoa zaidi ya 14 ili Majaji hawa wakasikilize kesi hizi. Kwa hiyo, naomba nilihakikishie Bunge lako tukufu kwamba kwenye Mahakama kesi hizi zinasikilizwa na kasi imeongezeka ndio maana backlogs zimebaki asilimia nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, anataka kufahamu kama watu hawa waliokaa zaidi ya miaka mitano wanaweza wakafidiwa. Taratibu za kisheria na principles za kesi kwamba pale ambapo unaona kwamba mashtaka haya yamekamilika na unaona ulibambikiziwa kesi na imechukua muda mrefu unaweza kurudi Mahakamai kufungua kesi ya madai.